Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Eriksson kutofundisha Ivory Coast

Wakala wa Sven-Goran Eriksson amesema kocha huyo hatochukua nafasi ya kuifundisha timu ya taifa ya Ivory Coast katika Kombe la Dunia.

Chama cha Soka cha Ivory Coast tayari kimesema walifanya mazungumzo na kocha huyo wa zamani wa England kwa ajili ya kuijaza nafasi hiyo.

Kocha huyo raia wa Sweden alikutana na viongozi wa Ivory Coast wiki iliyopita lakini hakuna makubaliano yaliyofikiwa.

Wakala wake Athole Still amesema "Sidhani kama Eriksson anahitaji kazi hiyo ya kuifundisha Ivory Coast. Natumai hatafundisha soka wakati huo wa Kombe la Dunia".

Wakala huyo alithibitisha walikutana na viongozi wa soka wa Ivory Coast, lakini walikwenda kuangalia mechi waliyocheza na Korea Kusini na kukutana na viongozi tu hakuna jingine.

Ivory Coast kwa sasa inamuwinda Mholanzi Guus Hiddink kuinoa timu yao kwa ajili ya Kombe la Dunia mwezi Juni nchini Afrika Kusini.

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Login Form