Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Pienaar afungiwa kuendesha gari

Steven Pienaar wa Everton amefungiwa kuendesha gari kwa kipindi cha muda wa miezi 12 baada ya kukiri aliendesha gari akiwa amekunywa pombe.

Kiungo huyo wa Everton alitolewa ndani ya gari na polisi wa Merseyside alfajiri ya tarehe 21 mwezi wa Februari baada timu yake kuichapa manchester United mabao 3-1 .

Mchezaji huyo raia wa Afrika Kusini alikutwa amekunywa pombe kwa kiwango cha mara mbili zaidi ya kiwango kinachokubalika wakati alipofanyiwa kipimo cha pumzi na polisi wa Liverpool.

Pienaar, mwenye umri wa miaka 27 alipigwa faini ya paundi 1,000 za Uingereza na mahakama ya Liverpool.

Pia ametakiwa kulipa faini nyingine zaidi ya paundi 100 kutokana na kushindwa kufuata sheria za barabarani.

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Login Form