Man U waitandika Arsenal 3-1
Hadi kipindi cha mapumziko Man U walikuwa wanaongoza kwa 3-0.
Kipa wa Arsenal Manuel Almunia alijifunga, Wayne Rooney akaongeza la pili na Ji-Sung Park la tatu.
Mnamo kipindi cha pili, Arsenal walijaribu kutimua vishindo kiasi cha kujipatia kifuta jasho kupitia mlinzi Vermaelen.
Katika mechi za awali Manchester City waliitandika Portsmouth 2-0, mabao ambayo yalifungwa na Emmanuel Adebayor pamoja na Vincent Kompany.
Portsmouth wanashikilia mkia kwenye ligi kuu huku matatizo ya fedha pia yakiendelea kuwazonga.
| Comments |
|
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
Powered by !JoomlaComment 3.26

