Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni
Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini Dar es salaam kesho kujadili mikakati ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka huu, ili waweze kuwahoji wagombea watafanya nini katika kutatua kero zao.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake nchini (Tamwa), Ananilea Nkya, katika taarifa iliyoyolewa kwa vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam.
Katika taarifa hiyo, Nkya, alisema kuwa miongoni mwa kero kubwa zinazorudisha nyuma maendeleo ya wananchi hasa wanawake ni mfumo usioridhisha wa elimu ambao unachangia idadi kubwa ya wanafunzi kutopata elimu bora na kuwepo kwa ongezeko kubwa la mimba shuleni.
Aliitaja kero nyingine sugu kuwa ni idadi kubwa ya vifo vya wanawake vinavyoweza kuzuilika vinavyotokana na ujauzito kwani hivi sasa wanawake zaidi ya 26 hufariki dunia kila siku hapa nchini kutokana na matatizo yanayoweza kuzuilika iwapo huduma za afya zitaboreshwa.
Tatizo jingine kubwa linalokabili wanawake na wanaume wengi alisema ni kipato duni ambapo kwa njia moja au nyingine huchangia kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Mkutano huo utakaofanyika katika ofisi za Tamwa, Sinza Mori, jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 4:00 asubuhi ambapo wahariri watajadili pia umuhimu wa wapiga kura kupambana na rushwa kwenye uchaguzi ili taifa liweze kupata viongozi makini na waadilifu kuharakisha maendeleo ya wananchi.
Tafiti zinaonesha kuwa rushwa kwenye uchaguzi ndicho chanzo kikubwa cha taifa kupata viongozi waroho, wanaojilimbikizia mali, wasiokuwa na uwezo na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi na taifa lao.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
JK aahidi kuanzisha programu ya malisho Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete,...
-
Kesi ya Mramba ya nguruma Kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia hasara serikali...
-
Maelfu wajitokeza kumuaga Kalumuna Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwemo watu wenye ulemavu jana...
-
CCM yazuia wagombea kushiriki midahalo TBC CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewazuia wagombea wake wa ubunge kushiriki...
-
Mchungaji amfyeka vidole mtoto kanisani MTOTO wa kike aliyetajwa kwa jina la Anna Danken (17) wa KijijiĀ ...
-
ZEC yaanza kusilikiza pingamizi mgombea CUF Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), imeanza kusikiliza rufaa ya mgombea...
-
JK: Vyama vya upinzani vya msimu MGOMBEA urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete ameviponda vyama vya upinzani...
-
Profesa Baregu avamiwa garini Mwenyekiti wa kamati ya kampeni ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo...
-
Mikoa 14 kukumbwa na ukame Baa la njaa linainyemelea Tanzania kutokana na utabiri wa hali ya...
-
Gari la mkuu wa kampeni Chadema lavunjwa vioo MWENYEKITI wa Kamati ya Kampeni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo...
-
Walimu mbaroni wizi wa mitihani ya darasa la sab WALIMU wakuu na wasimamizi wa mitihani, wanashikiliwa na polisi na...
-
Mahakama: Chenge ana kesi ya kujibu Mahakama ya wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam imesema mgombea...
-
Vyama 15 vyasaini rasimu ya mwongozo wa maadili Z`bar Viongozi wa vyama 15 vya siasa jana walisaini rasimu ya mwongozo...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Europe
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Advertisement Plan
- Australia
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Man Utd ushindi sasa basi
- Ratiba ya Ligi Kuu Uingereza 2010/2011
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Japan

