Thursday, September 09, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Uchunguzi wa vifo Duisburg waanza

Waendesha mashitaka nchini Ujerumani, wameanza kuchunguza chanzo cha vifo vya watu 19 katika msongamano uliosababisha kukanyagana uliotokea kwenye tamasha la muziki la Love Parade katika mji wa Duisburg. Watu 342 walijeruhiwa katika msongamano

huo uliotokea siku ya Jumamosi.

Akizungumza na waandishi habari katika mji wa Bayreuth, Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel alisema lazima uchunguzi wa kina ufanyike kubaini kilichosababisha maafa hayo.

Hapo jana gazeti la Ujerumani la Spiegel liliripoti katika mtandao wake kuwa waandalizi wa tamasha hilo walipewa kibali cha kuruhusu watu 250,000 kuhudhuria badala ya milioni 1.4 ambao walihudhuria. Mwandalizi wa tamasha hilo, Rainer Schaller alisema tamasha hilo halitafanywa tena kwa heshima ya wahanga wa maafa hayo na familia zao.

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form