Wednesday, September 08, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Obama na Cameron wakutana

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron amekanusha kwamba jitihada za ushawishi zilizofanywa na kampuni ya mafuta ya BP zilichangia uamuzi wa kuachiwa huru mripuaji wa ndege ya Pan Am katika eneo la Lockerbie, Scottland mwaka 1988, Abdel Baset al

-Megrahi. Shambulio hilo lililofanywa na raia wa Libya liliwaua watu 279.

Bwana Cameron alikuwa akizungumza wakati wa mkutano wake na Rais Barack Obama wa Marekani mjini Washington. Viongozi hao wawili walilaani kuachiwa kwa al-Megrahi mwaka uliopita.

Hata hivyo, Cameron amekataa wito wa kufanyika uchunguzi na badala yake amewaagiza wasaidizi wake kubaini iwapo taarifa zozote mpya kuhusu uamuzi huo zinatakiwa kutangazwa hadharani. Tatizo la kuvuja mafuta ya kampuni ya BP katika Ghuba ya Mexico, pia lilijadiliwa.

Waziri huyo mkuu wa Uingereza alisema anaelewa hasira iliyonayo Marekani kuhusu kuvuja mafuta hayo, lakini akaongeza kuwa kitendo cha kampuni ya BP kubakia imara na thabiti kina maslahi kwa nchi zote mbili.

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form