Jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria lahitaji bilioni 4/-
Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, unahitaji jumla ya Shilingi bilioni nne (sawa na dola milioni 3.7 za Marekani) kwa ajili ya ujenzi wa jengo la ofisi na makazi ya kudumu ya balozi.
Ubalozi huo tayari umepatiwa notisi ya kunyang’anywa eneo kwa kushindwa kuliendeleza.
Hayo yalielezwa na Balozi Msuya Mangachi, mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipotembelea ubalozi huo uliopo jijini Abuja juzi kukagua eneo la kiwanja cha ofisi na kisha kuonana na watumishi wa ubalozi huo.
Balozi Mangachi alisema serikali ya nchi hiyo imeipatia Serikali ya Tanzania eneo la kujenga ofisi za ubalozi lenye ukubwa wa mita za mraba 5,294 na eneo jingine la kujenga makazi ya balozi lenye ukubwa wa mita za mraba 2,500 na kwamba tangu mwaka 1995 halijaendelezwa kwa sababu ya kukosa fedha za ujenzi.
Hata hivyo, Serikali ya Tanzania imeshatoa dola 80,000 za Marekani kwa ajili ya kujenga uzio ili eneo hilo lisichukuliwe.
Pia alimweleza Waziri Mkuu kwamba maeneo ambayo Tanzania inaweza kunufaika kwa kushirikiana na nchi ya Nigeria ni sekta ya elimu, kilimo, ufugaji samaki wa mapambo, biashara, michezo hasa soka na utengenezaji wa filamu.
Akitoa mfano, alisema Serikali ya Afrika Kusini imepata walimu wengi kutoka Nigeria wa masomo ya sayansi na Kiingereza lakini ni baada ya kuwafuata na kuwasaili nchini kwao (Nigeria) ili kubaini uhalisi wa vyuo walivyotoka na uhalali wa vyeti vyao.
Akizungumzia kuhusu fursa za kibiashara na Wanigeria, Balozi Mangachi alisema kuna fursa kubwa ya biashara kwa sababu wakazi wake hawalimi kwa kiasi kikubwa na kila kitu wanaagiza kutoka nje ya nchi yao hasa baada ya kugundua wana biashara kubwa ya mafuta.
“Pia kipato cha mtu wa kati ni kikubwa ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika,” aliongeza.
Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema kuna haja ya kuangalia uwezekano wa kupata walimu kutoka Nigeria kama ambavyo Afrika Kusini imenufaika kwa sababu Tanzania bado inakabiliwa na uhaba wa walimu hata katika vyuo vya kufundishia walimu hao.
Kuhusu kilimo, Waziri Mkuu alisema bado Tanzania inakabiliwa na changamoto ya kuinua hadhi ya zao la muhogo ili uweze kupata soko zuri duniani.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

