Mwalimu aliyefariki aendelea `kula` mshahara, apanda cheo
Halmashauri ya wilaya ya Bunda, imeingia kwenye kashfa kubwa baada ya kubainika kumlipa mshahara mwalimu aliyekufa mwaka 2007.
Aidha, mwalimu huyo pia alipandishwa daraja mwaka 2009 na mshahara wake haijulikani unachukuliwa na nani .
Kashfa hiyo iliyoibuliwa juzi kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani na kuwaacha wajumbe wakiwa wameduwaa, inazidi kuonyesha wazi kuwa tume iliyopita kuhakiki watumishi hewa haikufanya kazi kama ilivyotarajiwa.
Akizungumza katika kikao hicho, diwani wa Kata ya Kibara, Venance Kamonyore, alisema anashangazwa na kitendo cha ofisi ya
Mkurugenzi kuendelea kupokea mshahara wa marehemu mwalimu Charles Mwijarubi aliyekuwa akifundisha katika Shule ya Msingi Namibu, Kata ya Kibara ambaye alikufa mwaka 2007.
“Niliwahi kumuuliza Mkurugenzi inakuwaje mtu amekufa mwaka 2007 mshahara wake unaendelea kuja mpaka sasa, la kushangaza mwaka 2009, alipandishwa daraja na mshahara kuongezeka...ndugu zake wanataka kujua nani anachukua fedha zao,” alihoji diwani.
Alisema ndugu zake walikuwa tayari kwenda wizarani kudai fedha hizo na ufisadi wa kutumia jina la marehemu kujipatia fedha ambazo familia yake hazijazipata.
“Toka nimeongea na Ded, sijapata majibu. Hivi kweli fedha hizo zinarudishwa Hazina na kwa nini jina hilo liendelee kuonekana kama yuko kazini wakati alishafariki dunia sasa ni mwaka wa nne,” alizidi kuhoji.
Hoja hiyo iliyosisimua baraza ilimfanya Mkurugenzi Mtendaji, Cyprian Oyier, kujitutumua kuijibu, akikiri kuwa aliambiwa na diwani na kufuatilia ili jina hilo liondolewe na mshahara usije.
“Nilimweleza ahakikishe wanawaandikia Hazina jina hilo liondolewe, yuko hapa atajibu kama mshahara huo unakwenda wapi, maana kama jina halijaondolewa utaendelea kuja,”alisema Mkurugenzi.
Hata hivyo Kaimu Mweka Hazina, Stella Msangya, hakuweza kujibu tuhuma hiyo mpaka mwisho wa kikao hali ambayo inazidisha mashaka juu ya tuhuma hiyo iliyoibuliwa ghafla.
Kaka wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina moja la mwalimu mstaafu Wijarubi, akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alisema wao wanafuatilia kuona ufisadi huo wa kutumia majina ya marehemu kupata fedha.
Alidai kuwa mpaka risti za mishahara ya Januari, mwaka huu ipo na wanayo na kuwa mrithi wa mali za marehemu ambaye ni kijana wake, James Mwijarubi, alimfikia diwani Februari, mwaka huu baada ya kupata taarifa na katika ufuatiliaji walibaini ukweli wa mambo.
Baadhi ya madiwani walisikitishwa na mchezo huo ambao walidai ni kashfa kubwa kwa halmashauri huku wakidai kuwa tume zinazoundwa kuchunguza watumishi hewa hazijazaa matunda kwa kuwa majina hewa bado yapo sekta za elimu na afya.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

