Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Tanroads yaanzisha mchakato wa mradi wa mabasi ya kasi

Hatimaye Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), umetangaza nia ya kutekeleza mradi wa magari ya mwendo kasi kwa kutangaza tenda kwa ajili ya kumpata mkandarasi atakayejenga barabara zitakazotumiwa na magari hayo.

Tangazo la tenda ya mradi huo lililotolewa jana na Tanroads lilieleza kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi itahusisha upanuzi wa barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Magomeni.

Lilieleza kuwa kipande hicho chenye urefu wa kilometa 10.9 kitahusisha ujenzi wa vituo 15 vikubwa vya magari, vituo viwili vya magari na madaraja mawili ya waenda kwa miguu.

Tangazo la tenda hiyo lilifafanua kuwa utekelezaji wa mradi huo utahusisha pia ujenzi wa vipande vya barabara kutoka Magomeni hadi Kivukoni, Magomeni hadi Morocco na Fire hadi Kariakoo.

Tanroads katika tangazo lake hilo imeeleza kuwa barabara hizo zitahusisha ujenzi wa vituo 14 vya magari, kituo kimoja cha magari hayo, daraja la waenda kwa miguu na kwamba mkandarasi atatakiwa kuzingatia miundombinu ya maji na huduma za mawasiliano.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, kazi hiyo itatekelezwa kwa miezi 24 baada tu ya mshindi kutangazwa.

Mradi wa magari ya mwendokasi unatazamiwa kuwa utasaidia kupunguza foleni jijini Dar es Salaam na kumaliza adha ya usafiri kwa wakazi wa Jiji.

 

CHANZO: NIPASHE
Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form