Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

RCO atoa ushahidi kesi ya wizi NMB

Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa kipolisi wa Ilala (RCO), Duani Nyanda (49), ametoa ushahidi wake katika kesi ya wizi wa zaidi ya Sh. milioni 234 mali ya benki ya NMB tawi la Mwanga mkoani Kilimanjaro na kueleza jinsi walivyoweza kuwatia mbaroni washtakiwa watano.

Nyanda ambaye ni shahidi wa 18, alikuwa akitoa ushahidi wake jana mbele ya jopo la mahakimu watatu, Penterine Kente, Aziza Temu na John Nkwabi wanaosikiliza kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.

Akiongozwa na wakili wa serikali Kanda ya Arusha, Juma Ramadhani, alidai kuwa mnamo Julai 11 mwaka 2007 alipata taarifa kuwa kuna majambazi wamevamia benki hiyo.

Alidai kuwa aliitwa na mkuu wake wa kazi kwa wakati huo, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana, ambaye alimtaka kuungana na askari wengine kwa ajili ya kufanya upelelezi wa tukio hilo.

Alidai baada ya kufika aliungana na askari wa upelelezi wa Wilaya ya Mwanga na Moshi na kuanza upelelezi ambapo simu ya mmoja wa mtu aliyeuwawa na polisi kwa kupigwa risasi akidhaniwa ni jambazi raia wa Kenya, Peter Mbungua, ndio iliwawezesha kuwapata baadhi ya washtakiwa.

Alidai katika simu hiyo waliangalia mtu aliyewasiliana na marehemu mara ya mwisho na kukuta ni mtu aitwaye Brenda, mkazi wa Arusha, ambapo waliomba kukutana naye.

Alidai kuwa Brenda aliwaeleza polisi kuwa alifahamiana na marehemu huyo kupitia mshtakiwa wa 11, Juliana Musanza, ambaye alimsaidia kupata simu ya kiganjani, ambapo walikwenda nyumbani kwake Julai 20, mwaka 2007.

Alidai baada ya kufika nyumbani kwa mshtakiwa wa 11, waliwakuta mshtakiwa, Devota Musanza ambapo katika kuwahoji waliwapeleka mahali wanapoishi mshtakiwa wa kwanza na wa pili katika eneo la Njiro mkoani Arusha.

Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa baada ya kufika katika nyumba hiyo majira ya usiku waliizingira hadi saa 12 alfajiri ndipo alipoaanza kuishambulia kwa kuwataka washtakiwa hao wajisalimishe.

Alidai washtakiwa hao walianza mashambulizi baada ya kushtuka kuwa polisi wamezingira nyumba hiyo na kulazimika kuomba msaada wa askari zaidi kwa kikosi cha Arusha.

Alidai walipambana na washtakiwa hao baada ya kurusha mabomu ya machozi na risasi, ambapo mshtakiwa Elizabeth alijisamilisha na kueleza kuwa ndani ya nyumba hiyo kuna watu wengine wawili.

Alidai walifanikiwa kuwakamata mshtakiwa wa kwanza, Samwel Saitoti na wa pili, Peter Kimani, ambapo baada ya kuwapekua waliwakuta wamevaa nguo za kuzuia risasi, silaha ya za kivita mbili aina ya SMG moja ikiwa na risasi 50 na nyingine risasi 26.

Pia alidai kuwa walikutwa na bastola 5 na mshtakiwa wa kwanza alikuwa na dola za Kimarekani 8,145 huku mshtakiwa wa pili akiwa na sh milioni 1.7.

Kesi hiyo inaendeleo leo ambapo shahidi huyo anaendelea kutoa ushahidi wake.

 

CHANZO: NIPASHE
Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form