Benki ya Dunia yatoa mikopo ya nyumba ya Sh50 bilioni
BENKI ya Dunia (WB) imeidhinisha Tanzania kupatiwa mkopo wa dola za Marekani 40 milioni sawa na zaidi ya Sh52 bilioni ili kufanikisha mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa kwa ajili ya Watanzania wenye kipato cha chini.
Benki hiyo, iliidhinisha fedha hizo mjini Washington, Marekani jana na kueleza kwamba zimetolewa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (Ida).
Chombo hicho cha fedha duniani kilisambaza taarifa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mradi huo utajenga nyumba za kisasa ili Watanzania wa kipato cha chini ambao mara nyingi wamekuwa wakishindwa kupata mikopo benki kwa sababu hawana mali isiyohamishika.
"Lengo la mradi huo ni kuwajengea uwezo wananchi, kuwawezesha kumiliki na kuishi kwenye nyumba bora," inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Msukumo mwingine wa kuidhinisha mabilioni hayo,
Taarifa hiyo, inaeleza kwamba benki ya dunia, iliidhinisha fedha hizo, kwa sababu wakazi wengi katika maeneo ya mijini, wanakabiliwa na matatizo ya makazi.
Inaeleza kwamba watu wengi wana matatizo ya makazi kutokana na kasi kubwa ya ongezeko la watu mjini na kusababisha ujenzi wa makazi holela bila kufuata utaratibu kwenye maeneo ambayo hayajapimwa.
"Kwa kuupa uwezo mradi wa ujenzi wa makazi, mkopo huu utawezesha wananchi uwezo wa kujiajiri wenyewe, kuongeza nafasi za ajira na hatimaye kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini," alisema Mkurugenzi wa WB katika nchi za Uganda, Burundi na Tanzania, John Murray McIntire kwenye hafla ya kuidhinisha fedha hizo.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

