Marekani yaonya wingi wa bidhaa feki nchini
BALOZI wa Marekani nchini , Alfonso Lenhardt amesema biashara ya bidhaa na dawa feki iliyoshamiri katika nchi za Afrika Mashariki ni hatari kwa uchumi wa nchi hizo pamoja na afya za wananchi wake.
Balozi huyo aliyasema hayo jana wakati akifungua warsha ya siku mbili ya kutoa mafunzo juu ya namna ya kupambana na bidhaa feki kwa maofisa wa taasisi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa jumuiya hiyo wanaohusika na kupamba na bidhaa hizo.
Kwa mujibu wa balozi huyu, biashara hizi mbali na kuhatarisha afya za watumiaji, pia zinasababisha nchi kukosa mapato ambayo yangetokana na kodi na pia wananchi kukosa kazi.
Katika hatua nyingine, Naibu Mkurugenzi wa Tume ya ushindani nchini Gregory Ndanu alisema katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, tume hiyo iliteketeza bidhaa feki zenye thamani ya Sh2 bilioni.
"Hawa wafanyabiashara wa bidhaa bandia wao wanachojali ni faida tu, mambo ya afya ya mtumiaji hawajui, kuteketeza hizi bidhaa inasaidia sana kwa sababu wengine hata wameshafilisika kutokana na bidhaa zao kuteketezwa," alisema Ndanu.
Ndanu ambaye pia alikuwa mshiriki katika semina hiyo iliyoandaliwa na Ubalozi wa Marekani nchini alisema ili kuimaliza biashara hiyo, lazima kuwe na bunge imara, mahakama imara, polisi wanaofuata sheria pamoja na maofisa wa forodha wanaofuata sheria katika ukaguzi.
"Hali ilivyo hivi sasa siyo imara, kuna matatizo katika ukaguzi wa bidhaa pamoja na ucheleweshwaji wa kesi katika mahakama zetu," alisema Ndanu.
Hata hivyo alisema katika Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanzania inaongoza na kupambana na tatizo hilo kwa kulinganisha na nchi nyingine wanachama wa jumuiya hiyo.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Mahakama: Chenge ana kesi ya kujibu Mahakama ya wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam imesema mgombea...
-
Vyama 15 vyasaini rasimu ya mwongozo wa maadili Z`bar Viongozi wa vyama 15 vya siasa jana walisaini rasimu ya mwongozo...
-
Mrufani aongezewa adhabu ya viboko Mahakama ya rufaa Tanzania imemuongea adhabu Mathias Mhagama, aliyepinga...
-
Tanesco yalalamikia vituo bandia vya Luku Shirika la Umeme nchini (Tanesco) limesema kuna ongezeko la vituo...
-
Chadema: Hatutaki siasa za maji taka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema hakina muda...
-
CCM na Chadema Moshi jino kwa jino Mkutano kati ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko...
-
Tendwa aiduwaza Chadema Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, ametupilia mbali pingamizi...
-
Chagueni viongozi pasipo kuangalia vyama-Mdee Mgombea ubunge wa jimbo la Kawe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo...
-
Wanawake wanaougua akili wananyanyasika Wanawake wanaougua ugonjwa wa akili, wananyanyasika kutokana na...
-
Slaa, Dk Bilal uso kwa uso Mwanza Mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),...
-
Mtihani darasa la saba wafanyika kwa utulivu Mtihani wa darasa la saba ulioanza jana kote nchini, ulifanyika katika...
-
Vurugu zaibuka Moshi, Iringa Watu watano wamekamatwa na Polisi mkoani hapa, wakihusishwa na vurugu...
-
Takukuru yapigwa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), imezidi kubanwa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Europe
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Advertisement Plan
- Australia
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Man Utd ushindi sasa basi
- Ratiba ya Ligi Kuu Uingereza 2010/2011
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Japan

