Marekani yaonya wingi wa bidhaa feki nchini
BALOZI wa Marekani nchini , Alfonso Lenhardt amesema biashara ya bidhaa na dawa feki iliyoshamiri katika nchi za Afrika Mashariki ni hatari kwa uchumi wa nchi hizo pamoja na afya za wananchi wake.
Balozi huyo aliyasema hayo jana wakati akifungua warsha ya siku mbili ya kutoa mafunzo juu ya namna ya kupambana na bidhaa feki kwa maofisa wa taasisi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa jumuiya hiyo wanaohusika na kupamba na bidhaa hizo.
Kwa mujibu wa balozi huyu, biashara hizi mbali na kuhatarisha afya za watumiaji, pia zinasababisha nchi kukosa mapato ambayo yangetokana na kodi na pia wananchi kukosa kazi.
Katika hatua nyingine, Naibu Mkurugenzi wa Tume ya ushindani nchini Gregory Ndanu alisema katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, tume hiyo iliteketeza bidhaa feki zenye thamani ya Sh2 bilioni.
"Hawa wafanyabiashara wa bidhaa bandia wao wanachojali ni faida tu, mambo ya afya ya mtumiaji hawajui, kuteketeza hizi bidhaa inasaidia sana kwa sababu wengine hata wameshafilisika kutokana na bidhaa zao kuteketezwa," alisema Ndanu.
Ndanu ambaye pia alikuwa mshiriki katika semina hiyo iliyoandaliwa na Ubalozi wa Marekani nchini alisema ili kuimaliza biashara hiyo, lazima kuwe na bunge imara, mahakama imara, polisi wanaofuata sheria pamoja na maofisa wa forodha wanaofuata sheria katika ukaguzi.
"Hali ilivyo hivi sasa siyo imara, kuna matatizo katika ukaguzi wa bidhaa pamoja na ucheleweshwaji wa kesi katika mahakama zetu," alisema Ndanu.
Hata hivyo alisema katika Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanzania inaongoza na kupambana na tatizo hilo kwa kulinganisha na nchi nyingine wanachama wa jumuiya hiyo.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

