Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Sumatra: Hali ya biashara ya usafirishaji abiria mbaya

Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema hali ya biashara ya usafirishaji abiria nchini ni mbaya kutokana na wamiliki kushindwa kuiendesha kwa ufanisi na kwa weledi.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Israel Sekirasa, wakati akizungumza na wadau wa utoaji wa huduma ya usafiri mijini.

Alisema hali ya utoaji wa huduma ya usafiri wa abiria kwa miji mikubwa kama Jiji la Dar es Salaam, hairidhishi kabisa kutokana na utaratibu wa wamiliki kuwasimamia madereva na makondakta wao.

Alisema hali hiyo huchangia katika kutofuata na kuvunja sheria na kanuni za usalama barabarani pamoja na utoaji huduma ya usafiri hafifu.

Alisema katika muundo wa makampuni yenyewe yanakuwa na wakaguzi wao ambao pamoja na kudhibiti matumizi mabaya ya magari yao, hudhibiti pia uvujaji wa mapato ya kampuni.

“Hali ilivyo sasa ni mbaya kutokana na kuwa na wamiliki wengi ambao wanashindwa kuendesha biashara ya usafirishaji kwa ufanisi na weledi, lazima tuboreshe mfumo wa utoaji huduma kupitia makampuni machache ambayo yanakuwa na uwezo wa kutoa huduma bora na mabasi yenye viwango,” alisema Sekirasa.

Alisema hali hiyo itasaidia pande zote mbili kwanza kwa wamiliki kufanya biashara ya usafirishaji kwa weledi na kwa ufanisi zaidi na kwa mdhibiti kuwasimamia watoa huduma wachache hivyo kuimarisha shughuli za udhibiti na hivyo kuwa na usafiri bora na salama kwa Watanzania.

 

CHANZO: NIPASHE
Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form