Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Ndege ya ATCL yapata hitilafu angani

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), juzi ilikwamisha safari ya maofisa kadhaa waandamizi wa serikali waliokuwa wakienda mkoani Tabora kuhudhuria kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Ndege hiyo iliondoka jijini Dar es Salaam juzi ikiwa imewachukua maofisa hao wa serikali, lakini ililazimika kurudi njiani baada ya kupata matatizo ya kiufundi wakati ikiwa angani.

Baadhi ya maofisa hao wa serikali (majina tunayo) waliozungumza na Nipashe jana, walithibitisha ndege hiyo kupatwa na hitilafu wakati ikiwa angani na hivyo, kulazimika kukatisha safari na kurejea jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATC, William Haji, alipoulizwa jana na Nipashe alisema tatizo lililoisibu ndege hiyo halikuwa kubwa kama linavyokuzwa.

Kama kungekuwapo na hitilafu ningejua, lakini kama lilikuwapo, ni mambo ya kurekebishika tu,” alisema Haji.

Alisema kilichotokea kwa ndege hiyo, ni kuchelewa muda wa kwenda mkoani Kigoma, ambao mwisho wake ni saa 9:00 alasiri, jambo ambalo lililazimisha safari hiyo kusitishwa kwa vile kuna tatizo la taa za uwanjani.

Hata hivyo, alisema siku hiyo hiyo, ndege hiyo ilikwenda mkoani Mwanza, kwa kuwa uwanja wake una taa na jana ilikwenda Kigoma na kuongeza kuwa mzigo wa gharama za kuwahifadhi abiria waliokwama kusafiri, ulibebwa na shirika.

Maadhimisho hayo, ambayo kilele chake kilihitimishwa katika uwanja wa mpira wa Ali Hassan Mwinyi, mkoani humo, yaliyohutubiwa na Rais Jakaya Kikwete.


CHANZO: NIPASHE
Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form