IGP Mwema apangua jeshi la Polisi, ahamisha vigogo wa juu
MKUU wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema amefanya tena mabadiliko ya uongozi kwenye jeshi hilo, lakini safari hii akitupia jicho zaidi kwenye Kikosi cha Usalama Barabarani na maofisa wa vitengo, kikiwemo cha habari.
Mabadiliko hayo ya viongozi wa Kikosi cha Usalama Barabarani yamekuja siku chache baada ya Mwema kufanya mabadiliko makubwa ya makamanda wa mikoa katika kipindi ambacho wimbi la ujambazi linaonekana kuanza kurejea kwa kasi.
Msemaji mkuu wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Abdallah Mssika alisema jana kuwa katika mabadiliko mapya, Mwema amemteua Kamishna Msaidizi Mohammed Mpinga kuwa kamanda mpya wa Kikosi cha Usalama Barabarani badala ya Kamishna Msaidizi Mwandamizi James Kombe ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.
Kamanda Mssika alisema kuwa nafasi ya Kamanda Mpinga inachukuliwa na mkuu wa usalama barabarani mkoani Pwani, Mrakibu Mwandamizi Johansen Kahatano. Kabla ya uteuzi huo, Kamanda Mpinga alikuwa ni afisa mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani.
Katika mabadiliko hayo, Mwema amemteua Mrakibu Msaidizi Advera Senso kuwa msemaji msaidizi wa polisi badala ya Mrakibu Suzan Kaganda, ambaye amehamishiwa Kanda ya Dar es Salaam kuwa msaidizi wa kitengo cha masuala ya operesheni.
Wengine waliohamishwa ni ofisa mnadhimu wa mkoa wa Tanga, ACP Simon Mgawe ambaye anakwenda makao makuu ya Polisi, wakati mkuu wa usalama barabarani mkoani Kigoma, SSP Salehe Mbaga anakwenda kuwa mkuu mpya wa usalama barabarani mkoa wa Pwani.
Kamanda Mssika alisema kuwa mkuu wa upelelezi wa Kikosi cha Reli, Mrakibu Adolphina Kapufi sasa anakuwa ofisa mnadhimu wa mkoa wa Tanga na nafasi yake inachukuliwa na SP Sebastian Mbutta kutoka upelelezi mkoani Singida.
Alisema SP Robert Masanja, ambaye ni mkufunzi Chuo cha Polisi CCP Moshi, sasa anakuwa mkuu wa polisi wilayani Songea mkoani Ruvuma. Awali nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na ASP Marco Joshua ambaye sasa anahamishiwa ofisi ya kamanda wa mkoani Ruvuma.
Kamanda Mssika aliwataja maafisa wengine waliohamishwa kuwa ni ASP Anthony Masonzu, anayetoka makao makuu ya Kikosi cha Usalama Barabarani kwenda makao makuu ya Polisi wakati mkuu wa kitengo hicho mkoani Kigoma, Mrakibu Msaidizi William Mkonda ameteuliwa kukaimu nafasi ya mkuu wa kitengo hicho mkoani Kigoma.
Kamanda Mssika alisema kuwa mabadiliko hayo ni ya kawaida na yanalenga zaidi katika kuboresho ufanisi katika kutoa huduma za polisi kwa jamii.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

