Mvua yaleta madhara, yabomoa nyumba 175 Mwanza
NYUMBA 175 zimeanguka kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali kunyesha usiku wa kuamkia juzi na kusababisha vifo vya watu wanne akiwemo mtoto wa umri wa miaka sita huku familia 86 zikikosa makazi.
Nyumba hizo zilibomolewa na mvua hiyo katika Kijiji cha Kisesa, Kijiji cha Matale, Kijiji cha Ihishi, na Kiseke na kwamba nyumba 21 zilianguka Kisesa kilicho wilayani Magu na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi mmoja.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kaimu kamanda wa polisi wa mkoa, Monosius Komba aliwataja watu waliofariki katika kijiji hicho kuwa ni Marthar Samweli, 25, na Yunus Peter, 25, wakati Freeman alijeruhiwa na kulazwa Hospitali ya Sekou Toure.
Komba alisema kuwa katika Kijiji cha Ihishi, nyumba 119 zilizokuwa zimejengwa kwa matofali ya tope zilianguka usiku huo na kusababisha familia 86 kukosa makazi na mtu mmoja kujeruhiwa.
Komba alimtaja majeruhi aliyeangukiwa na nyumba kuwa ni Sophia Changaa, 26, ambaye hali yake inaendelea vizuri baada ya kupata matibabu.
Alisema kuwa vijiji vingine ambavyo vilipata madhara ya mvua hiyo na kusababisha nyumba kuanguka ni pamoja na Kisesa kilicho wilayani Ilemela ambako nyumba 30 zilinguka lakini hakukuwa na madhara, wakati nyumba tatu zilianguka katika Kijiji cha Matale kilicho Kata ya Sangabuye.
Komba alisema kuwa katika kijiji cha Kiseke B wilayani Ilemela, nyumba moja ya Charles Kishorogo, 45, ilianguka majira ya saa 10:00 usiku na kusababisha kifo cha mtoto mmoja aliyetambulika kwa jina la Wankumu Kirari, 6, wakati katika wilaya mpya ya Busweru mtu moja aliyetambulika kwa jina la Mashauri Masasira, 60, aliangukiwa na nyumba yake na kufariki papo hapo.
Kamanda Komba alisema kuwa tathmini ya athari za maafa bado inafanyiwa kazi na taarifa za maafa hayo zitatolewa baadaye na kwamba watu waliobomokewa na nyumba zao wamepewa hifadhi katika shule za sekondari na msingi.
Mjini Mwanza, mvua hizo zilisababisha maji kujaa kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza kutokana na mkondo wa Mto Kimilabagalu ambao ulifurika maji yaliyotoka maeneo ya karibu na mto huo.
Akizungumza na waandishi wa habari kaimu meneja ,Mchunguzi Byantao alisema mvua hiyo ilinyesha muda mfupi na kusababisha uwanja huo kujaa maji.
Kaimu meneja wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Daniel Njenga aliwaambia waandishi wa habari kuwa kujaa kwa uwanja huo kunatokana na mkono wa mto huo kupitia hapo na kushindwa kudhibitiwa ili usiweze kuingiza maji uwanjani.
Alisema kila mvua zinaponyesha na maji kutoka mto huo yamekuwa yakiingia na kujaa katika eneo la uwanja na hivyo kuufanya kuwa katika mazingira ambayo si mazuri kwa ndege kutua na hivyo kuiomba serikali kuangalia uwezekano wa kudhibiti mto huo.
Mvua hizo zilianza kunyesha Machi 7 na kusababisha athari kubwa ikiwemo kujaa maji na kusabaisha uwanja huo kufungwa kwa muda juzi.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

