Maalim Seif aendelea kupumzishwa zaidi hospitalini
HALI ya katibu mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad inaendelea vizuri, lakini bado hajaruhusiwa kutoka hospitalini na watu hawaruhusiwi kumuona kwa kile kilichoelezwa na msaidizi wake, Jussa Ismail Jussa kuwa ni kumpa muda wa kupumzika na kuwa karibu na daktari.
Maalim Seif amelazwa Hospitali ya Hindu Mandal iliyo jijini Dar es Salaam tangu Ijumaa baada ya kuugua ghafla ugonjwa wa mkamba (bronchitis), ambao hutokana na kuvimba kwa njia za hewa, baada ya mapafu kushambuliwa na vijidudu.
Alikumbwa na ugonjwa huo akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere akisubiri kupanda ndege ambayo ingempeleka Muscat, Oman.
Juzi mganga wa mwanasiasa huyo, Dk Kaushik Ramaiya alisema kuwa hali ya Maalim Seif ilikuwa inaendelea vizuri na kwamba angeruhusiwa kuondoka hospitalini jana tofauti ya matarajio ya awali ambayo yalikuwa siku nne.
Lakini jana, baada ya Mwananchi kufika hospitalini hapo saa 4:00 asubuhi na kukutana na mganga wake, Dk Kaushik Ramaiya, ilielezwa kuwa kiongozi huyo wa upinzani visiwani Zanzibar ataendelea kuwa hospitalini hapo.
Dk Kaushik, hata hivyo, alieleza kuwa hali ya Maalim Seif inaendelea vizuri, lakini bado wanaendelea kumuangalia hadi kesho (leo).
"Bado hatujamruhusu, tumemshauri aendelee kupumzika lakini anaendelea vizuri sana," alisema Dk Kaushik.
Alifafanua kuwa Maalim Seif huenda akaruhusiwa kuanzia leo, kwa kuwa hali yake imeendelea kuimarika kutokana na vipimo na dawa alizopata hospitalini hapo.
Naye msaidizi wake wa karibu, Ismail Jussa, ambaye pia ni mbunge wa kuteuliwa wa CUF na msaidizi wa karibu wa Maalim Seif, ilielezwa kuwa mwanasiasa huyo ataendelea kuwa hospitalini hapo licha ya hali yake kuendelea kutengemaa.
Jussa alisema hali ya Maalim Seif inaendelea vizuri na kwamba hawatamruhusu mwandishi yeyote kuingia kumuona kiongozi huyo mkongwe wa siasa za Tanzania.
"Maalim anaendelea vizuri, lakini bado hajaruhusiwa anaendelea kupumzika na kwa leo (jana) hatumruhusu mwandishi yeyote kumuona," alisema Jussa.
Alisema kwa sasa amezuiliwa dawa zote zinazotumia na kwamba tiba yake inahusisha vidonge tu.
Jussa alisema: "Tumeamua kudhibiti watu kumuona kwa sababu, jana (juzi) tuliwaruhusu na Maalim Seif akazungumza nao... sidhani kama kutakuwa na jipya la kumuuliza, alisema.
Alisema hata daktari wake ameridhika na maendeleo ya afya yake na kwamba huenda akamruhusu leo, baada ya kumuangalia.
Jussa ambaye aliteuliwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete kuwa mbunge, alisema Maalim Seif anahitaji muda mzuri wa kupumzika ili kurahisisha kuimarika kwa afya yake.
"Kwanza leo (jana) mtamuuliza nini, kama ni kuongea alishaongea kwa kweli kama mnampenda mwacheni apumzike, anahitaji muda huo kwa sasa," alisema Jussa.
Kuugua ghafla kwa Maalim Seif kulisababisha uvumi kuzuka na kuenea kwa kasi jijini Dar es salaam na visiwani Zanzibar zikidai kuwa mkongwe huyo wa siasa amefariki, hali iliyomlazimu aongee na waandishi kukanusha habari hizo.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

