Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Vigogo wa Rites waanza kutimka

WAKATI serikali ikitarajiwa kutoa tamko la mustakabali wa shirika mahututi la reli, TRL kesho, tayari mameneja wa kampuni ya Rites ya India inayoendesha shirika hilo wameanza kutimka kurejea kwao.

Rais Jakaya Kikwete alidokeza juzi wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kuwa hatma ya shirika hilo muhimu na kongwe nchini itajulikana kesho baada ya kufanyika kwa mazungumzo, lakini hakufafanua kauli yake.

Lakini Mwananchi imedokezwa kuwa vigogo watatu wa TRL wameshatimka na kurejea kwao India hata kabla ya kutangazwa kwa uamuzi wa mwisho juu ya shirika hilo lililokuwa likiendesha huduma ya usafiri wa reli kati ya Dar es salaam na mikoa ya Kati na Kanda ya Ziwa.

Vyanzo vya uhakika vya habari vilithibitishia gazeti hili kuondoka kwa mameneja hao ambao uongozi wao umekumbwa na kikwazo kikubwa kutoka kwa wafanyakazi wa shirika hilo ambao wamekuwa wakiendesha migomo mara kwa mara.

Hata hivyo, Naibu Waziri wa Miundombinu Hezekiah Chibulunje hakutaka kuthibitisha au kukanusha taarifa za kuondoka kwa vigogo hao na badala yake akawataka wananchi kusubiri ahadi ya rais kesho.

"Mheshimiwa rais ameshasema; mimi nikisema kitu hapa itakuwa ni utovu wa nidhamu. Tusubiri ahadi ya rais aliyotoa kwamba kila kitu kitajulikana Alhamisi," alifafanua Chibulunje.

Alipoulizwa maendeleo ya mchakato wa serikali kununua hisa asilimia 51 za Rites, alijibu: "Nafikiri haitakuwa sahihi Rais kazungumza jana mimi nizungumze leo, subiri alhamisi ikipita njoo."

Mpashaji wa habari hizo aliiambia Mwananchi akisema: "Mameneja watatu wameondoka kurejea India; wamechoka na mambo yalivyo sasa... serikali inahaha kununua hisa lakini majadiliano ya bei bado yanaendeleo."

Kwa mujibu wa chanzo hicho, kikao cha Baraza la Mawaziri ndicho kinasubiriwa kupata mwafaka wa pamoja kuhusu hatua ambayo inapaswa kupigwa na serikali katika kipindi hiki.

Mkataba kati ya Rites, inayomiliki asilimia 51 ya hisa za TRL, na serikali yenye hisa asilimia 49, ulisainiwa Oktoba 2007 na ni wa miaka 25, lakini umekuwa ukikumbwa na matatizo kadhaa ya kiuendeshaji.

CHANZO MWANANCHI

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form