Mrema adai Spika Sitta amlipe Sh 1 bilioni
HATIMAYE mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema ameanza rasmi mchakato wa kumfikisha mahakamani spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samwel Sitta baada ya kumwandikia barua ya kumtaka amuombe radhi na kumlipa fidia ya Sh 1bilioni.
Mrema amefikia uamuzi huo siku mbili tu tangu atangaze kusudio la kumshtaki mahakamani kiongozi huyo wa Bunge ambaye alimuelezea Mrema kuwa ni mtu aliyefilisika kisiasa na kifedha na kufikia hatua ya kusema kuwa anapewa fedha na CCM ili aipigie debe.
Sitta alizungumza hayo baada ya Mrema kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kumtuhumu spika huyo kuwa ana makundi kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano na kwamba anakiuka sheria na taratibu za Bunge kwa kuendelea kuzungumzia suala la kashfa ya Richmond nje ya chombo hicho cha kutunga sheria.
Lakini majibu ya Sitta yalimfanya Mrema angake na kuamua kuweka hadharani kiasi cha akiba ya fedha alichonacho kwenye akaunti yake ya benki na kutishia kuwa atampeleka spika huyo mahakamani iwapo atashindwa kutoa ushahidi wa tuhuma zake.
"Mheshimiwa Samwel Sitta Spika wa Bunge la Tanzania, nakuarifu rasmi kwamba nakusudia kukufungulia kesi ya madai kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania kutokana na kauli zako ulizozitoa magazetini dhidi yangu," anasema Mrema ambaye aliwahi kuwa mbunge wa jimbo la Vunjo kwa tiketi ya CCM na baadaye Temeke kwa tiketi ya NCCR Mageuzi.
Katika barua yake hiyo yenye kumbukumbu namba TLP/HQ/SIR/03/55 ya Machi 8 mwaka huu, Mrema amempa Spika Sitta siku saba amuombe radhi katika magazeti yaliyomnukuu kwa uzito ulele na kumlipa fidia hiyo katika muda huo.
Akizungumza na Mwananchi jana kwenye ofisi za makao makuu ya TLP yaliyo Magomeni akiwa ameshika barua hiyo, Mrema alisema: "Spika alikaririwa na magazeti akisema kuwa mimi Mrema ni mhuni, nimepitwa na wakati, pia nimefilisika kisiasa na kipesa... sasa ninatafuta njia ya kujinasua katika hali hiyo.
"Katika gazeti jingine alisema kuwa kuna uwezekano kuwa nimepata pesa ili niipigie debe CCM; gazeti jingine akasema kuwa Mrema ni muhu
Mrema, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani alisema kuwa, kauli za Sitta zimemdhalilisha mbele ya jamii akiwa kama Mwenyekiti wa TLP hali iliyosababisha wanachama 500,000 wa chama hicho nchini wakose imani naye.
"Nikiwa mwenyekiti wa TLP, chama cha nne kwa ukubwa nchini, kauli za Sitta hazivumiliki amenikashifu na kunitukana, wanachama wa TLP wamekosa imani na mimi kutokana na kauli hizo, "alisema Mrema.
"Pia kauli zako zimenivunjia heshima niliyojijengea katika utumishi wangu uliotukuka serikalini ambako nilifanya kazi kwa zaidi ya miaka 30 nikiwa ofisa usalama wa taifa, mbunge, waziri na baadaye Naibuwa Waziri Mkuu."
Mrema alisema kuwa kauli hizo za Sitta zimemuathiri kwa kuwa ameshajitangaza kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo kwa kuwa kauli hizo zinaweza kutumiwa na wapinzani wake kummaliza kisiasa.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

