Wanaougua fistula waomba msaada
Wanawake wanaougua ugonjwa wa Fistula, wameiomba serikali kuwawekea matibabu kila mkoa ili kuwasaidia kupata huduma kwa urahisi kwa kuwa inawagharimu kiasi kikubwa cha fedha kusafiri hadi jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, mmoja wa wagonjwa huo ambaye amelazwa katika Hospitali ya CCBRT, Paulina Chaula (34), Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, alisema kumekuwepo na tatizo kubwa la ukosefu wa huduma hiyo katika mikoa mbalimbali nchini.
Alisema kuwa alipata ugonjwa huo alipojifungua mtoto wa nane na tatizo hilo lilimsumbua kwa mwaka mmoja na miezi mitatu.
Chaula alisema baada ya kuugua kwa muda mrefu, ndipo alipopatiwa taarifa kuwa huduma hiyo inatolewa katika CCBRT na ndipo alipoamua kuitafuta.
Aidha alisema fistula imekuwa ni ugonjwa ambao huwaletea madhara makubwa kwa wanawake ikiwemo kutokufanya kazi nzito, kuachwa na wanaume.
Aliiomba serikali kutoa msaada kwa wanawake ambao wameathirika na ugonjwa huo ili waweze kupatiwa matibabu.
Mratibu wa masuala ya Ufundi wa Uzazi katika Hospitali hiyo, Dk. Brenda D'emerlo, alisema katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana, madaktari wanawake walijitolea kutibu ugonjwa huo bure na hata kuwafariji baadhi wa wagonjwa.
Aidha, lisema kuwa ugonjwa huo unaweza kutoweka endapo tu kutakuwa na huduma bora katika suala zima la uzazi wa mpango ikiwemo na kumjali mama anapokuwa mjamzito.
Daktari wa magonjwa ya wanawake katika hospitali hiyo, Vindhya Pakirama, alisema ugonjwa huo hutibiwa kwa muda wa wiki mbili au mwezi.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

