Mke wa Balozi auawa kinyama na shamba boi
Mke wa Balozi mwandamizi mstaafu wa Tanzania nchini Marekani, Andrew Daraja, ameuawa kinyama kwa kuchomwa kisu cha kifuani sehemu ya titi la kushoto na polisi wanamtafuta mhudumu wa shamba, James Mabakuri (22), kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga, alimtaja mke huyo wa balozi kuwa ni Anna Daraja, mkazi wa Kimara Temboni, jijini Dar es Salaam.
Kamanda Kalinga aliiambia Nipashe kuwa mauaji hayo yalitokea juzi nyumbani kwa Balozi Daraja Temboni, jijini Dar es Salaam wakati balozi akiwa safarini mkoani Tanga.
Kamanda Kalinga alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye wanaendelea kumtafuta, mara baada ya tukio hilo anadaiwa kuiba kiasi ya Sh. milioni 2 na kutoweka nazo bila kuchukua kitu kingine.
Akisimulia zaidi tukio hilo, Kamanda Kalinga alisema Februari 14, mwaka huu Balozi Daraja alimuaga mke wake kuwa anasafiri kwenda Muheza, Tanga na kumuacha na mhudumu wa shamba ambaye alikuwa akiishi kwenye nyumba hiyo.
Alisema wakati Balozi Daraja akiwa safarini, kijana huyo anadaiwa kuwa alimchoma Anna kisu kwenye titi la kushoto na kufa papo hapo.
Alisema mtuhumiwa baada ya kuhakikisha mama huyo amekufa alianza kufanya upekuzi kwenye nyumba hiyo, ikiwemo chumbani kwa balozi.
Alisema mtuhumiwa huyo mara baada ya kuzikuta fedha hizo sehemu zilipokuwa zimehifadhiwa, alitoweka eneo la tukio na kwenda kusikojulikana.
“Nyumba hiyo ilikuwa na vitu vyenye thamani kubwa, lakini inaelekea mtuhumiwa hakuwa na nia navyo, alichukua fedha na kutokomea nazo,” alisema Kamanda Kalinga.
Kamanda Kalinga alisema kuwa upekuzi uliofanywa kwenye chumba cha mtuhumiwa kilichopo nje ya nyumba kubwa ya balozi huyo kulikutwa nguo za aina mbalimbali pamoja na vitu vingine. Alisema nguo hizo ni mali ya mtuhumiwa.
Alisema uchunguzi wa awali uliofanyika kwenye nyumba hiyo, umebaini kuwa mtuhumiwa huyo alifanya kitendo hicho cha kikatili usiku kutokana na mazingira waliyoyakuta.
“Tukio hili lingefanyika mchana huyu mama angepata msaada, lakini inaonyesha wazi kuwa mtuhumiwa alimvizia usiku ndipo akafanya mauaji hayo,” alisema Kamanda Kalinga.
Alisema juhudi za kumsaka mtuhumiwa huyo katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam na nje ya mkoa zinaendelea.
Kamanda Kalinga alisema mtuhumiwa huyo inadaiwa kuwa aliletwa na fundi ujenzi ambaye hajafahamika jina lake kwa ajili ya kazi alizokuwa akizifanya.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi zaidi.
Akizungumza kwa njia ya simu na Nipashe, Balozi Daraja alisema wakati wa tukio la kuuawa kwa mke wake alikuwa safarini mkoani Tanga.
“Jana (juzi) niliporudi nyumbani kutokea Tanga nilipofika kwenye geiti la nyumba yangu, niligonga muda mrefu bila mafanikio,” alisema.
Alisema mara baada ya kufanikiwa kuingia ndani (bila kuelezea aliingiaje), aliukuta mwili wa mke wake ukiwa umelala kwenye gereji huku kisu kikiwa kimechomwa kwenye titi.
Alisema hadi sasa hafahamu mtu aliyefanya kitendo hicho na kwamba uchunguzi unaendelea.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

