`Shule za binafsi zipunguze ada`
Wamiliki wa shule za binafsi nchini wameshauriwa kuangalia uwezekano wa kupunguza ada hasa katika kipindi hiki cha mtikisiko wa kiuchumi.
Kufuatia hali hiyo, baadhi ya wazazi wameshaonyesha kushindwa kulipa ada kwa kuwahamisha watoto wao kuotoka shule za Kingereza na kuwarudisha kwenye shule za serikali kufuatia mtikisiko wa kiuchumi.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Shule za Binafsi za Sekondari Kanda ya Dar es Salaam, Kiramu Mbowe, wakati wa maadhimisho ya siku ya Jumiya ya Madola ambayo huadhimishwa Machi 8.
Alisema tayari mtikisiko wa kiuchumi umeshaonyesha matokeo kwenye sekta ya elimu kwani baadhi ya wazazi wameshaonekana wazi kushindwa kulipa ada kitu ambacho lazima wamiliki wa shule binafsi wajadili na kuona namna gani wanaweza kusaidia hasa katika upinguzaji wa ada.
Aidha, alisema maadhimisho ya Siku ya Madola inaweleta wanafunzi na walimu pamoja ambapo wanatumia mada huo kubadilishana mawazo.
Akifungua maadhimisho hayo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Gaudensia Kabaka, alishukuru uongozi wa shule ya Sekondari ya Shaaban Robert kwa kuandaa maadhimisho hayo ya kitaifa ambayo ni muhimu kwa wanafunzi na watu mbalimbali.
Alisema serikali itaendelea kuinua kiwango cha elimu nchini hasa kwenye upande wa sayansi na teknologia kwa kuongeza fedha kwa mwaka ujao wa fedha.
Makamu wa Rais wa Jumuya ya Madola, Andy Chande, aliwashukuru wazazi wa kuanza kufatilia maendeleo ya watoto wao tofauti na hapo awali walikuwa wakiwaachia walimu peke yao.
Chande alishukuru pia serikali kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu hasa kwa mpango wa kuongeza fedha kwa ajili ya kusapoti kauli mbiu ya mwaka huu.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
JK aahidi kuanzisha programu ya malisho Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete,...
-
Kesi ya Mramba ya nguruma Kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia hasara serikali...
-
Maelfu wajitokeza kumuaga Kalumuna Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwemo watu wenye ulemavu jana...
-
CCM yazuia wagombea kushiriki midahalo TBC CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewazuia wagombea wake wa ubunge kushiriki...
-
Mchungaji amfyeka vidole mtoto kanisani MTOTO wa kike aliyetajwa kwa jina la Anna Danken (17) wa KijijiĀ ...
-
ZEC yaanza kusilikiza pingamizi mgombea CUF Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), imeanza kusikiliza rufaa ya mgombea...
-
JK: Vyama vya upinzani vya msimu MGOMBEA urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete ameviponda vyama vya upinzani...
-
Profesa Baregu avamiwa garini Mwenyekiti wa kamati ya kampeni ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo...
-
Mikoa 14 kukumbwa na ukame Baa la njaa linainyemelea Tanzania kutokana na utabiri wa hali ya...
-
Gari la mkuu wa kampeni Chadema lavunjwa vioo MWENYEKITI wa Kamati ya Kampeni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo...
-
Walimu mbaroni wizi wa mitihani ya darasa la sab WALIMU wakuu na wasimamizi wa mitihani, wanashikiliwa na polisi na...
-
Mahakama: Chenge ana kesi ya kujibu Mahakama ya wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam imesema mgombea...
-
Vyama 15 vyasaini rasimu ya mwongozo wa maadili Z`bar Viongozi wa vyama 15 vya siasa jana walisaini rasimu ya mwongozo...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Europe
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Advertisement Plan
- Australia
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Man Utd ushindi sasa basi
- Ratiba ya Ligi Kuu Uingereza 2010/2011
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Japan

