`Shule za binafsi zipunguze ada`
Wamiliki wa shule za binafsi nchini wameshauriwa kuangalia uwezekano wa kupunguza ada hasa katika kipindi hiki cha mtikisiko wa kiuchumi.
Kufuatia hali hiyo, baadhi ya wazazi wameshaonyesha kushindwa kulipa ada kwa kuwahamisha watoto wao kuotoka shule za Kingereza na kuwarudisha kwenye shule za serikali kufuatia mtikisiko wa kiuchumi.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Shule za Binafsi za Sekondari Kanda ya Dar es Salaam, Kiramu Mbowe, wakati wa maadhimisho ya siku ya Jumiya ya Madola ambayo huadhimishwa Machi 8.
Alisema tayari mtikisiko wa kiuchumi umeshaonyesha matokeo kwenye sekta ya elimu kwani baadhi ya wazazi wameshaonekana wazi kushindwa kulipa ada kitu ambacho lazima wamiliki wa shule binafsi wajadili na kuona namna gani wanaweza kusaidia hasa katika upinguzaji wa ada.
Aidha, alisema maadhimisho ya Siku ya Madola inaweleta wanafunzi na walimu pamoja ambapo wanatumia mada huo kubadilishana mawazo.
Akifungua maadhimisho hayo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Gaudensia Kabaka, alishukuru uongozi wa shule ya Sekondari ya Shaaban Robert kwa kuandaa maadhimisho hayo ya kitaifa ambayo ni muhimu kwa wanafunzi na watu mbalimbali.
Alisema serikali itaendelea kuinua kiwango cha elimu nchini hasa kwenye upande wa sayansi na teknologia kwa kuongeza fedha kwa mwaka ujao wa fedha.
Makamu wa Rais wa Jumuya ya Madola, Andy Chande, aliwashukuru wazazi wa kuanza kufatilia maendeleo ya watoto wao tofauti na hapo awali walikuwa wakiwaachia walimu peke yao.
Chande alishukuru pia serikali kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu hasa kwa mpango wa kuongeza fedha kwa ajili ya kusapoti kauli mbiu ya mwaka huu.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

