Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Watu 40 wafa kwa mafuriko huko Madeira, Ureno

Maafisa wa Uoakoaji nchini Ureno, bado wanaendelea kuwasaka walionusurika, baada ya mafuriko na maporomoko kukumba kisiwa cha kitalii cha Madeira, siku ya Jumamosi. Watu 42 wanakisiwa wamekufa, huku wengine

120 wakiripotiwa kujeruhiwa.

Mamia ya wengine wameachwa bila ya makaazi, baada ya upepo mkali kuharibu madaraja, barabara na nyumba katika kisiwa hicho maarufu kwa watalii. Timu za madaktari zimeondoka katika mji mkuu wa Lisbon kuelekea katika kisiwa hicho kilichopo katika bahari ya Atlantic, huku maafisa wa Ureno wakihofia idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka.

Waziri Mkuu wa Ureno, Jose Socrates alitembelea eneo hilo la mkasa na kuahidi serikali itasaidia katika juhudi za msaada na ukarabati wa kisiwa hicho. Mafuriko hayo yanaripotiwa kuwa mabaya kabisa kuwahi kukumba kisiwa cha Madeira, tangu yale mafuriko ya mwaka 93, ambapo watu wanane walikufa.

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form