Skendo la Ununuzi wa Rada ya Tanzania, BAE Yapigwa Faini Dola Milioni 450
![]() Wakala wa ununuzi wa rada ya Tanzania, Shailesh Vithlani |
Skendo la ununuzi wa rada ya ulinzi ya Tanzania toka kwa kampuni ya BAE Systems ya Uingereza limechukua sura nyingine nchini Uingereza kwa kampuni ya BAE kupigwa faini ya dola 450 kwa kukiri kutumia rushwa kukamilisha madili yake. |
|
| Kampuni ya BAE System iliyoiuzia rada ya ulinzi Tanzania imepigwa faini ya jumla ya dola Milioni 450 (Zaidi ya Tsh. Bilioni 580) kwa kutumia rushwa katika kukamilisha dili zake na Tanzania, Jamhuri ya Cheki, Hungary na Saudi Arabia. Awali taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai (SFO) ya Uingereza iliipa mwezi mmoja BAE Systems kukiri makosa yake au kufikishwa mahakamani Awali SFO iligundua kuwa mkataba wa ununuzi wa rada wa mwaka 1999, kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Uingereza ya BAE Systems uligubikwa na rushwa kubwa. Ununuzi wa rada hiyo ulifanikishwa na wakala Shailesh Vithlani ambaye aliifanya Tanzania itoe TSh bilioni 16 zaidi ya bei halisi katika ununuzi wa rada hiyo. Vithlani inasemekana alipewa dola milioni 12 (zaidi ya TSh. bilioni 12) kama kamisheni ya kufanikisha dili hilo na inasemekana aligawana pesa hizo na maafisa saba wa ngazi za juu katika serikali ya Tanzania. Vithlani alitoroka Tanzania miaka mitatu iliyopita akiwa nje kwa dhamana baada ya kufunguliwa mashtaka na alikamatwa mwaka jana nchini Uswizi alikokuwa akijificha. Mbali na rushwa kutumika katika ununuzi wa rada ya Tanzania, BAE pia ilituhumiwa kutumia rushwa katika kukamilisha uuzaji wa ndege moja ya kijeshi kuiuzia nchi ya Afrika Kusini na uuzaji wa ndege nyingine ya kijeshi ambao haukufanikiwa kwa Jamhuri ya Cheki. "Kampuni ya BAE inajutia yaliyotokea na inakubali kubeba mzigo kwa matatizo yaliyotokea", alisema mwenyekiti wa BAE, Dick Olver. BAE ilikiri kuwa malipo ya kamisheni kwa mtekelezaji wa dili la rada ya Tanzania hayakuwekwa wazi kama ilivyotakiwa na kwasababu hiyo BAE imekubali kutoa paundi milioni 30 ambazo baadhi ya pesa hizo zitatumika kwaajili ya manufaa ya Tanzania. Mkurugenzi wa SFO, Richard Alderman alielezea kufurahishwa kwake na makubaliano yaliyofikiwa na kuongeza kuwa huo ndio utakuwa mwisho wa uchunguzi wao kwa kampuni ya BAE. |
||
| Comments |
|
|
||||||||||||
Powered by !JoomlaComment 3.26
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria lahitaji bilioni 4/- Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, unahitaji jumla ya Shilingi bilioni...
-
Mwalimu aliyefariki aendelea `kula` mshahara, apanda cheo Halmashauri ya wilaya ya Bunda, imeingia kwenye kashfa kubwa baada...
-
EAC kujenga mtandao wa reli Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeazimia kujenga mtandao wa...
-
Tanroads yaanzisha mchakato wa mradi wa mabasi ya kasi Hatimaye Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), umetangaza nia ya kutekeleza...
-
RCO atoa ushahidi kesi ya wizi NMB Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa kipolisi wa Ilala (RCO), Duani Nyanda...
-
Ngeleja: Serikali kununua Dowans ndoto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amekanusha vikali kwamba...
-
Kikwete Rais wa kwanza kutia mguu Kitunda Ziara ya Rais Jakaya Kikwete kwenye kata ambayo haijawahi kutembelewa...
-
Ikulu lawamani vita ya ufisadi RIPOTI ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mpango wa Kutathmini Utawala...
-
Jaji Bomani kutopambana na Rais Kikwete 2010 BAADA ya kutajwa kuwa na dhamira ya kumvaa Rais Jakaya Kikwete, kwenye...
-
Kapuya, Tucta washangaana SERIKALI imesema inafanya uchunguzi kujua sababu zilizofanya Shirikisho...
-
Benki ya Dunia yatoa mikopo ya nyumba ya Sh50 bilioni BENKI ya Dunia (WB) imeidhinisha Tanzania kupatiwa mkopo wa dola za...
-
Watu 3,000 wapiga simu kujua kama Maalim Seif amekufa ZAIDI ya watu 3,800 wamepiga simu kutoka kona mbalimbali duniani kwa...
-
Marekani yaonya wingi wa bidhaa feki nchini BALOZI wa Marekani nchini , Alfonso Lenhardt amesema biashara ya bidhaa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- Advertisement Plan
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- United States
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Europe
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Google now in Tanzania, Advertise!
- Australia
- Henry Joseph Shindika aula
- Vyeti feki - Mawaziri sita wanasa
- United Kingdom


