Uingereza Kuzibania Viza Za Wanafunzi
Serikali ya Uingereza imetangaza kuweka sheria na masharti magumu katika utolewaji wa viza za uanafunzi.
Waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza, Alan Johnson amesema kuwa masharti magumu yameongezwa katika maombi ya viza za uanafunzi kwa wanafunzi toka nchi zote duniani.
Mojawapo ya masharti yaliyoongezwa katika uombaji wa viza za uanafunzi ni kwa mwanafunzi anayeomba viza kutakiwa awe anaongea kiingereza fasaha.
Miongoni mwa sheria ziliongezwa ni kama vile kuwazuia wanafunzi wenye viza za muda mfupi kuwaleta Uingereza jamaa zao kama vitegemezi (dependant) wao.
Sheria mpya zimewekwa kufuatia waziri mkuu wa Uingereza kutaka masharti ya utolewaji wa viza yaangaliwe upya kufuatia tukio la mwanafunzi wa Nigeria aliyemaliza masomo yake nchini Uingereza kujaribu kuilipua ndege ya Marekani bila mafanikio.
Sababu kubwa ya kuwekwa kwa sheria hizi ni kupunguza idadi ya wanafunzi toka barani Afrika na Asia ambao hujishughulisha zaidi na kufanya kazi kuliko masomo yao.
Awali mwaka mmoja uliopita Uingereza iliongeza ugumu katika utolewaji wa viza za wanafunzi kwa kuwataka wanafunzi watoe vithibitisho vya kuweza kujilipia ada yote ya masomo yao na pia kuwa na uwezo wa kifedha kukimu gharama za maisha yao nchini Uingereza.
Wiki iliyopita, Uingereza ilisimamisha kwa muda kupokea maombi ya viza za wanafunzi kutoka maeneo ya kaskazini mwa India, Nepal na Bangladesh. Hatua hiyo ilitokana na idadi kubwa kuliko kawaida ya maombi ya viza za uanafunzi toka maeneo hayo.
Wizara ya mambo ya ndani ya Uingereza imesema kuwa kutokana na masharti mapya ya utolewaji wa viza za wanafunzi, idadi ya wanafunzi watakaopewa viza itapungua sana lakini hata hivyo wizara hiyo ilikataa kutoa tathmini zao.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Kura za Rais kutangazwa majimboni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema kuwa matokeo ya Rais yatatangazwa...
-
Mhandisi apata wakati mgumu mbele ya JK Mhandisi wa Maji mkoani hapa, Mkama Bwire, juzi alipata wakati mgumu...
-
Sumatra: Hali ya biashara ya usafirishaji abiria mbaya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini...
-
Watu 600 hawana makazi Mwanza Familia zaidi ya 120 zenye takribani watu 600 hazina makazi kutokana...
-
Mramba aibuka kwa mapadri, masheikh Mbunge wa Rombo, Basil Mramba (CCM), amekutana na viongozi wa dini...
-
Ndege ya ATCL yapata hitilafu angani Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), juzi ilikwamisha safari...
-
IGP Mwema apangua jeshi la Polisi, ahamisha vigogo wa juu MKUU wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema amefanya tena...
-
Mvua yaleta madhara, yabomoa nyumba 175 Mwanza NYUMBA 175 zimeanguka kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo...
-
Maalim Seif aendelea kupumzishwa zaidi hospitalini HALI ya katibu mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif...
-
Zenji washerehekea kurejea kwa umeme WANANCHI wa visiwa vya Zanzibar walikuwa ni wenye furaha baada ya...
-
Vigogo wa Rites waanza kutimka WAKATI serikali ikitarajiwa kutoa tamko la mustakabali wa shirika...
-
Mrema adai Spika Sitta amlipe Sh 1 bilioni HATIMAYE mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema...
-
Rufaa ya mgombea binafsi ngoma nzito Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amewaandikia barua maprofesa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- Advertisement Plan
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- United States
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Europe
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Google now in Tanzania, Advertise!
- Australia
- Henry Joseph Shindika aula
- Vyeti feki - Mawaziri sita wanasa
- United Kingdom

