Mafundi ujenzi wafa kwa kufunikwa kifusi D`Salaam
Mafundi ujenzi wawili wakazi wa Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam, wamekufa papo hapo baada ya kufunikwa na kifusi cha mchanga walichokuwa wakikichimba.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi eneo la Pugu Bagdad.
Kamanda Shilogile alisema mafundi hao ambao ni James Katenga (27) na Adamu Mtolela (30), walikutwa na umauti huo wakati wakiendelea na uchimbaji mchanga kwenye moja ya machimbo yaliyopo eneo hilo.
Wakati huohuo, dereva wa pikipiki Mussa Issah (24), amekufa papo hapo na abiria wake kujeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na gari dogo aina ya Audi Saloon eneo la Brush lililopo barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Liberatus Sabas, alisema ajali hiyo ilitokea juzi eneo hilo wakati gari hilo lenye namba za usajili T 357 ASE likiendeshwa na Magreth Lega (34).
Alisema gari hilo lilikuwa alikitokea eneo la Kamata kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati dereva wa pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 391 AYU alikuwa akitokea Tazara kuelekea Kamata.
Kamanda Sabas alimtaja aliyejeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Gidmash Geofrey (22), ambaye amelazwa hospitali ya Temeke kwa matibabu na dereva wa gari hilo anashikiliwa na polisi wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Kura za Rais kutangazwa majimboni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema kuwa matokeo ya Rais yatatangazwa...
-
Mhandisi apata wakati mgumu mbele ya JK Mhandisi wa Maji mkoani hapa, Mkama Bwire, juzi alipata wakati mgumu...
-
Sumatra: Hali ya biashara ya usafirishaji abiria mbaya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini...
-
Watu 600 hawana makazi Mwanza Familia zaidi ya 120 zenye takribani watu 600 hazina makazi kutokana...
-
Mramba aibuka kwa mapadri, masheikh Mbunge wa Rombo, Basil Mramba (CCM), amekutana na viongozi wa dini...
-
Ndege ya ATCL yapata hitilafu angani Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), juzi ilikwamisha safari...
-
IGP Mwema apangua jeshi la Polisi, ahamisha vigogo wa juu MKUU wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema amefanya tena...
-
Mvua yaleta madhara, yabomoa nyumba 175 Mwanza NYUMBA 175 zimeanguka kutokana na mvua kubwa iliyoambatana na upepo...
-
Maalim Seif aendelea kupumzishwa zaidi hospitalini HALI ya katibu mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif...
-
Zenji washerehekea kurejea kwa umeme WANANCHI wa visiwa vya Zanzibar walikuwa ni wenye furaha baada ya...
-
Vigogo wa Rites waanza kutimka WAKATI serikali ikitarajiwa kutoa tamko la mustakabali wa shirika...
-
Mrema adai Spika Sitta amlipe Sh 1 bilioni HATIMAYE mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema...
-
Rufaa ya mgombea binafsi ngoma nzito Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amewaandikia barua maprofesa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- Advertisement Plan
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- United States
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Europe
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Google now in Tanzania, Advertise!
- Australia
- Henry Joseph Shindika aula
- Vyeti feki - Mawaziri sita wanasa
- United Kingdom

