Shahidi kesi ya Liyumba ashindwa kutoa ushahidi
MKURUGENZI wa ukaguzi wa miradi kutoka Wizara ya Fedha na Uchumi, Amir Mcharo jana aliiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu asitoe ushahidi katika kesi inayomkabili kigogo wa zamani wa Benki Kuu (BoT), Amatus Liyumba kwa madai kuwa anasumbuliwa na shinikizo la damu.
Mcharo, 48, ambaye ni shahidi wa tisa wa upande wa mashtaka alitoa ombi hilo jana mbele ya jopo la mahakimu watatu linaloongozwa na Edson Mkasimongwa mara baada ya kuapishwa na kupanda kizimbani tayari kwa kutoa ushahidi.
Liyumba anakabiliwa na kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh221 bilioni wakati wa mradi wa ujenzi wa majengo ya ghorofa pacha yaliyo kwenye viwanja vya ofisi ya makao makuu ya BoT.
Mara baada ya kutoa ombi hilo, Hakimu Mkasimongwa alimuuliza shahidi huyo kuwa kama ugonjwa wake hautokani na msongo wa mawazo au hofu ya kutoa ushahidi.
Lakini shahidi huyo alikataa akisema kuwa huwa anasumbuliwa na ugonjwa huo mara kwa mara.
"Naomba nisitoe ushahidi leo (jana), kesho nikiwa najisikia vizuri nitakuja kutoa ushahidi wangu, "aliomba shahidi huyo.
Wakili wa Liyumba, Majura Magafu alidai kuwa kila mtu ana shinikizo la damu hivyo kwa kuwa shahidi huyo alishasimama kizimbani, akaapishwa hana budi kutoa ushahidi angalau kidogo.
Magafu alidai lazima ifike wakati upande wa mashtaka uelewe shahidi huyo anaposema ana shinikizo la damu kwa kuwa hata mteja wao ana magonjwa yake na bado yupo mahabusu.
Baada ya kutolewa kwa hoja hizo, Hakimu Mkasimongwa aliamuru leo upande wa mashtaka ufike mahakamani na mashahidi wao wote, akiwepo mkurugenzi huyo wa ukaguzi wa miradi.
CHANZO MWANANCHI
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria lahitaji bilioni 4/- Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, unahitaji jumla ya Shilingi bilioni...
-
Mwalimu aliyefariki aendelea `kula` mshahara, apanda cheo Halmashauri ya wilaya ya Bunda, imeingia kwenye kashfa kubwa baada...
-
EAC kujenga mtandao wa reli Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeazimia kujenga mtandao wa...
-
Tanroads yaanzisha mchakato wa mradi wa mabasi ya kasi Hatimaye Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), umetangaza nia ya kutekeleza...
-
RCO atoa ushahidi kesi ya wizi NMB Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa kipolisi wa Ilala (RCO), Duani Nyanda...
-
Ngeleja: Serikali kununua Dowans ndoto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amekanusha vikali kwamba...
-
Kikwete Rais wa kwanza kutia mguu Kitunda Ziara ya Rais Jakaya Kikwete kwenye kata ambayo haijawahi kutembelewa...
-
Ikulu lawamani vita ya ufisadi RIPOTI ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mpango wa Kutathmini Utawala...
-
Jaji Bomani kutopambana na Rais Kikwete 2010 BAADA ya kutajwa kuwa na dhamira ya kumvaa Rais Jakaya Kikwete, kwenye...
-
Kapuya, Tucta washangaana SERIKALI imesema inafanya uchunguzi kujua sababu zilizofanya Shirikisho...
-
Benki ya Dunia yatoa mikopo ya nyumba ya Sh50 bilioni BENKI ya Dunia (WB) imeidhinisha Tanzania kupatiwa mkopo wa dola za...
-
Watu 3,000 wapiga simu kujua kama Maalim Seif amekufa ZAIDI ya watu 3,800 wamepiga simu kutoka kona mbalimbali duniani kwa...
-
Marekani yaonya wingi wa bidhaa feki nchini BALOZI wa Marekani nchini , Alfonso Lenhardt amesema biashara ya bidhaa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- Advertisement Plan
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- United States
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Europe
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Google now in Tanzania, Advertise!
- Australia
- Henry Joseph Shindika aula
- Vyeti feki - Mawaziri sita wanasa
- United Kingdom

