Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

Shahidi kesi ya Liyumba ashindwa kutoa ushahidi

MKURUGENZI wa ukaguzi wa miradi kutoka Wizara ya Fedha na Uchumi, Amir Mcharo jana aliiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu asitoe ushahidi katika kesi inayomkabili kigogo wa zamani wa Benki Kuu (BoT), Amatus Liyumba kwa madai kuwa anasumbuliwa na shinikizo la damu.

Mcharo, 48, ambaye ni shahidi wa tisa wa upande wa mashtaka alitoa ombi hilo jana mbele ya jopo la mahakimu watatu linaloongozwa na Edson Mkasimongwa mara baada ya kuapishwa na kupanda kizimbani tayari kwa kutoa ushahidi.

Liyumba anakabiliwa na kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh221 bilioni wakati wa mradi wa ujenzi wa majengo ya ghorofa pacha yaliyo kwenye viwanja vya ofisi ya makao makuu ya BoT.

Mara baada ya kutoa ombi hilo, Hakimu Mkasimongwa alimuuliza shahidi huyo kuwa kama ugonjwa wake hautokani na msongo wa mawazo au hofu ya kutoa ushahidi.

Lakini shahidi huyo alikataa akisema kuwa huwa anasumbuliwa na ugonjwa huo mara kwa mara.

"Naomba nisitoe ushahidi leo (jana), kesho nikiwa najisikia vizuri nitakuja kutoa ushahidi wangu, "aliomba shahidi huyo.

Wakili wa Liyumba, Majura Magafu alidai kuwa kila mtu ana shinikizo la damu hivyo kwa kuwa shahidi huyo alishasimama kizimbani, akaapishwa hana budi kutoa ushahidi angalau kidogo.

Magafu alidai lazima ifike wakati upande wa mashtaka uelewe shahidi huyo anaposema ana shinikizo la damu kwa kuwa hata mteja wao ana magonjwa yake na bado yupo mahabusu.

Baada ya kutolewa kwa hoja hizo, Hakimu Mkasimongwa aliamuru leo upande wa mashtaka ufike mahakamani na mashahidi wao wote, akiwepo mkurugenzi huyo wa ukaguzi wa miradi.

CHANZO MWANANCHI

Comments
Add New Search
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form