Serikali yaandaa bajeti ya ziada
Serikali inakusudia kuongeza kiasi cha Sh. bilioni 19 katika bajeti yake ya mwaka huu ambacho pamoja na mambo mengine, kitatumika kusaidia sekta ya kilimo kwa kutoa mikopo kwa wakulima kupitia Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB).
Muswada wa kuidhinisha nyongeza hiyo ambao umepangwa kujadiliwa na wabunge kwa siku mbili mfululizo kuanzia leo, utaingizwa kwenye bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi.
“Itakumbukwa kuwa katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ya Agosti 21, mwaka 2008, alielekeza kwamba fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania, zitakazorudishwa serikalini ziingizwe katika mfuko mkuu wa Serikali kwa ajili ya matumizi ya shughuli za maendeleo ya nchi ikiwemo kuongeza fedha kwenye mfuko wa ruzuku ya mbolea,” inasomeka sehemu ya muswada huo.
Wakati huo huo, baadhi ya wafadhili wamejitoa kuchangia bajeti ya mwaka huu na wengine wamekataa kutoa kiasi chote cha fedha walichokuwa wameahidi.
Akitoa mwongozo wa bajeti ijayo bungeni jana, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, alisema Uholanzi imetangaza kusitisha msaada wake wa dola za Kimarekani milioni 40.
Alisema Uingereza imesitisha kutoa kiasi cha paundi milioni 10 ambazo ni zaidi ya Sh. bilioni 20 wakati Denki ya Dunia imesitisha mchango wa dola milioni 10.
Alisema hadi Desemba mwaka jana, Japan na Ujerumani hazikuwa zimetoa kiasi chochote cha ahadi zao kwenye bajeti ya Serikali.
Alisema wamesitisha kutoa fedha hizo kwa maelezo kuwa hawaridhishwi na juhudi za Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

