Serikali yaandaa bajeti ya ziada
Serikali inakusudia kuongeza kiasi cha Sh. bilioni 19 katika bajeti yake ya mwaka huu ambacho pamoja na mambo mengine, kitatumika kusaidia sekta ya kilimo kwa kutoa mikopo kwa wakulima kupitia Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB).
Muswada wa kuidhinisha nyongeza hiyo ambao umepangwa kujadiliwa na wabunge kwa siku mbili mfululizo kuanzia leo, utaingizwa kwenye bajeti ya Wizara ya Fedha na Uchumi.
“Itakumbukwa kuwa katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ya Agosti 21, mwaka 2008, alielekeza kwamba fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania, zitakazorudishwa serikalini ziingizwe katika mfuko mkuu wa Serikali kwa ajili ya matumizi ya shughuli za maendeleo ya nchi ikiwemo kuongeza fedha kwenye mfuko wa ruzuku ya mbolea,” inasomeka sehemu ya muswada huo.
Wakati huo huo, baadhi ya wafadhili wamejitoa kuchangia bajeti ya mwaka huu na wengine wamekataa kutoa kiasi chote cha fedha walichokuwa wameahidi.
Akitoa mwongozo wa bajeti ijayo bungeni jana, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, alisema Uholanzi imetangaza kusitisha msaada wake wa dola za Kimarekani milioni 40.
Alisema Uingereza imesitisha kutoa kiasi cha paundi milioni 10 ambazo ni zaidi ya Sh. bilioni 20 wakati Denki ya Dunia imesitisha mchango wa dola milioni 10.
Alisema hadi Desemba mwaka jana, Japan na Ujerumani hazikuwa zimetoa kiasi chochote cha ahadi zao kwenye bajeti ya Serikali.
Alisema wamesitisha kutoa fedha hizo kwa maelezo kuwa hawaridhishwi na juhudi za Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara.
| Comments |
|
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria lahitaji bilioni 4/- Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, unahitaji jumla ya Shilingi bilioni...
-
Mwalimu aliyefariki aendelea `kula` mshahara, apanda cheo Halmashauri ya wilaya ya Bunda, imeingia kwenye kashfa kubwa baada...
-
EAC kujenga mtandao wa reli Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeazimia kujenga mtandao wa...
-
Tanroads yaanzisha mchakato wa mradi wa mabasi ya kasi Hatimaye Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), umetangaza nia ya kutekeleza...
-
RCO atoa ushahidi kesi ya wizi NMB Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa kipolisi wa Ilala (RCO), Duani Nyanda...
-
Ngeleja: Serikali kununua Dowans ndoto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amekanusha vikali kwamba...
-
Kikwete Rais wa kwanza kutia mguu Kitunda Ziara ya Rais Jakaya Kikwete kwenye kata ambayo haijawahi kutembelewa...
-
Ikulu lawamani vita ya ufisadi RIPOTI ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mpango wa Kutathmini Utawala...
-
Jaji Bomani kutopambana na Rais Kikwete 2010 BAADA ya kutajwa kuwa na dhamira ya kumvaa Rais Jakaya Kikwete, kwenye...
-
Kapuya, Tucta washangaana SERIKALI imesema inafanya uchunguzi kujua sababu zilizofanya Shirikisho...
-
Benki ya Dunia yatoa mikopo ya nyumba ya Sh50 bilioni BENKI ya Dunia (WB) imeidhinisha Tanzania kupatiwa mkopo wa dola za...
-
Watu 3,000 wapiga simu kujua kama Maalim Seif amekufa ZAIDI ya watu 3,800 wamepiga simu kutoka kona mbalimbali duniani kwa...
-
Marekani yaonya wingi wa bidhaa feki nchini BALOZI wa Marekani nchini , Alfonso Lenhardt amesema biashara ya bidhaa...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- Advertisement Plan
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- United States
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Europe
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Google now in Tanzania, Advertise!
- Australia
- Henry Joseph Shindika aula
- Vyeti feki - Mawaziri sita wanasa
- United Kingdom

