Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
![]() |
Tatizo la wanaume kuwahi kufika kileleni mapema ambalo huzua hofu kwa wanaume wengi sana duniani kiasi cha wengine kwenda kwa waganga kutafuta tiba limepatiwa ufumbuzi baada ya dawa ambayo inasemekana inaongeza ufanisi mara tatu zaidi kuzinduliwa nchini Ufaransa. |
|
| Tatizo la wanaume kuwahi kufika kileleni mapema wakati wa kujamiiana ambalo huwatia hofu mamilioni ya wanaume wengi duniani limepatiwa dawa kwa mara ya kwanza. Tatizo hili huwanyima raha wanaume wengi kwani mwanaume anapowahi kufika kileleni mapema kabla ya mpenzi wake humwacha mwanamke akiwa bado hajafikia hitimisho la raha ya kujamiiana. Wanaume wenye tatizo hili ili wasiaibike kitandani mbele ya wapenzi wao wamekuwa wakihaha kutafuta dawa za kuwafanya waweze kuwaridhisha wapenzi wao, kuna wanaume wengine hufikia hatua za kwenda kwa waganga kutafuta tiba. Dawa za kutibu tatizo hilo zimezinduliwa kwenye kongamano la tatu la matibabu ya magonjwa ya jinsia linalofanyika nchini Ufaransa. Dawa hizo mpya ambazo zimepewa jina la "Priligy" zimetengenezwa kwa kutumia madawa ya Dapoxetine ambayo yamegundulika kuonyesha ufanisi mkubwa katika kuchelewesha mwanaume kufika kileleni mapema. Wanaume waliotumia dawa hizo wakati wa majaribio ufanisi wao kitandani unasemekana uliongezeka kwa mara tatu zaidi. Dawa hizo zimethibitishwa rasmi ufanisi wake na vyombo vya afya nchini Austria, Finland, Ujerumani, Italia, Hispania, Sweden na Ureno. Prof. Jacques Buvat wa taasisi iliyovumbua dawa hizo alisema kuwa dawa zinaweza zikatumiwa na wanaume wenye umri kati ya miaka 18 na 64 na hazina madhara yoyote katika kusimama kwa uume. Prof Buvat alisema kuwa wanaume wengi hufika kileleni kati ya dakika moja na dakika kumi. " Kwa wastani muda unaokubalika ni kati ya dakika nne na tano, wanaume wanaofika kileleni ndani ya dakika moja au chini ya dakika moja huhesabika wana tatizo la kufika kileleni mapema". "Tatizo la wanaume kuwahi kufika kileleni mapema huwatokea wanaume wengi zaidi kuliko tatizo la kusimama vyema kwa uume". "Wanaume wengi huwa hawapendi kuzungumzia tatizo hili na asilimia 40 ya wanaume hutumia pombe kama njia ya kutatua tatizo hilo" alisema. |
||
| Comments |
|
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
Powered by !JoomlaComment 3.26
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula


