Saturday, July 31, 2010
   
Text Size

Tafuta kwenye Website hii

CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya

Zamani ilikuwa ni wanaume waliokuwa wakilalamika, kwamba wake zao hawataki kuwapa chakula cha usiku kama wanavyotaka. Lakini baadae yaani siku hizi ni zamu ya wanawake kulalamika.

Katika nyumba nyingi siku hizi hasa mijini wanawake ndio wanolalamika zaidi kukosa chakula cha usiku kama wanavyotaka kutoka kwa waume zao.

Kwa nini hali hii?

Ukweli ni kwamba maisha yamebadilika sana na kila mtu anajitahidi sana kutaka kuhahakisha kwamba anafanya kazi hadi anaishiwa nguvu kabisa, akili na mwili vinachoka. Wanaume wengi wanaolalamikiwa na wake zao kuhusu kupata uhaba wa chakula cha usiku ni wale wanaofanya kazi sana.

Ningependa kuwashauri wanaume kwamba wakati wanafanya kazi zao mchana wakumbuke kwamba kuna wake zao wapendwa ambao wanawasubiri jioni kuzungumza nao na zaidi ya hapo. Wakumbuke hawajaoa kazi bali wameoa wake. Pamoja na kwamba ni muhimu kwao kufanya kazi, lakini wakumbuke kwamba kazi hazina mwisho.

Kuna jambo ambalo wanaume na hata wanawake hawalijui vizuri, hili ni lile linalohusu mazoezi. Mtu anapofanya mazoezi anawezesha damu kuzunguka na kufikia sehemu zote za mwili kwa kiwango kinachotakiwa. Kukaa ofisini kutwa na kurudi nyumbani na kukaa kwenye kochi na kuangalia TV siyo aina ya maisha inayoshauriwa tuishi. Mwili unapochangamka kwa damu kufika kila mahali kwa kiwango kinachotakiwa hamu ya kutoa chakula cha usiku na kukipokea huwa kubwa.

Lakini mbaya zaidi ni kwa wanawake wenyewe pia. Kuna wanawake ambao bado wanaishi kwa miiko ya karne moja nyuma. Hawa wanangoja wanaume zao wawachokoze, wasipofanya hivyo, basi hata mwaka watakaa wakilalamika kwamba hawapati chakula cha usiku. Tukumbuke kwamba hata wanaume nao ni binadamu pia, huhitaji wakati mwingine kushtuliwa, kwani wakishtua wao tu kila siku, kuna wakati hukinai.

Comments
Add New Search
Mwananchi mwenye Hasira  - Chakula cha Usiku   |133.51.86.xxx |2009-08-18 22:59:46
Duh, sijui mwandishi huyu ni mwanamke au mwanaume aliye katika ndoa na amefanya
uchunguzi kwa muda gani! Najiuliza maana ni kweli kabisa aliyowasilisha na kwa
kiwango kikubwa amenigusa mimi nikiwa mwanaume ambaye nakumbana na malalamiko ya
hivi na kunifanya kila ikifika muda wa kwenda home jioni, naanza kujiuliza
itakuwaje nikidaiwa mlo wa usiku na mke wangu maana najikuta mchovu mwili, akili
na mawazo! Nachukua sompo muhimu hapa KUFANYA MAZOEZI. Asante sana!
karavuze y  - Nimekubali mnatisha   |41.223.228.xxx |2009-08-24 12:15:51
Sina mengi zaidi ya kukwambia kuwa huo ni ukweli mtupu
jacqueline  - mama watatu   |196.45.46.xxx |2009-08-29 07:03:23
jamani umeongea ukweli kabisa, tena umesahua swala moja la lap top hili ndo
linawatia jeuri, kazi zote za ofcn wanazikumbuka kizifanyia nyumbani. kwa kweli
mila nazo zachangia ku2danganya wanawake ndo maana na vicheni party wanayapiga
vita eti ukimuanza mumeo mara kwa mara utaonekana malaya. hongera kwa mada.
Shangarai, N  - Mr.   |41.188.142.xxx |2009-09-03 05:19:45
Kwa kweli maisha yamebadilika sana na yanaendelea kubadilika kwa kasi ya
ajabu!
Cha msingi hapa ni kujijali.
pale mtu atakapoweza kujijali yeye
mwenyewe, ndipo ataweza kumjali mwenzie. Wenzetu wa dunia ya kwanza (US & UK
)wametushinda kwa hilo tu. Ukijijali, maana yake hautauchakaza mwili wako kwa
kuji-ovadozi kwa kazi zisizokwisha. Hivyo utapanga ratiba inayojali mambo
mengine na kama utaifuata, utaweza kufanya mazoezi, kupumzika na chakula cha
usiku itakuwa kama kawa!
sarah  - chakula cha usiku: wahanga sasa ni mwanawake!   |193.220.81.xxx |2009-09-08 04:35:11
Katika nyumba nyingi siku hizi hasa mijini wanawake ndio wanolalamika zaidi
kukosa chakula cha usiku kama wanavyotaka kutoka kwa waume zao.

Kwa
nini hali hii?
cuthbert  - Hi Sarah   |196.43.77.xxx |2009-09-23 12:43:44
Vp sarah? unajua wanaume tuna mambo mengi sana,so mwisho wa siku unaporudi home
na kumkuta mwenzako ana nguvu tele inakuwa ngumu wote kuridhishana
dont throw stone  - ukweli uko palepale   |196.46.108.xxx |2009-09-10 09:06:15
ni kweli kwamba mishe za maisha zinatushosha kiasi kwamba hataukirudi nyumbani
hutaki kusikia au kuona ... zaidi ya kulala.

Ukitaka kujua ukweli wa hii isu
tazama ongezeko la matangazo ya dawa za kuongeza nguvu za kiume - ndani na
kutoka nje za nje.
bety  - ni kweli hata mimi yananikuta   |196.46.120.xxx |2009-12-16 01:09:20
mimi na mume wangu wote tunafanya kazi serikalini na tunarudi wote jioni lakini
mwenzangu anadai amechoka hali hii huwa inaniumiza sana,upo sahihi mwandishi
bety  - NI NKWELI KABISA   |196.46.120.xxx |2009-12-16 01:10:13
NI KWELIIIIIIIIIIIIIII
alex  - wote hamjui   |80.72.105.xxx |2010-01-06 07:18:06
tatizo wanawake hawajui kutega kwa mfan o ukinitegea wakati narudi nyumbani
nikakukuta mtupu umekaa kwenye dressing table halafu nikjaribu kukuvamia unaweka
mapozi mpaka nikubembembeleze we unafikiri ukinipa kitatokea nini
itakua tamu
we acha tu ukitaka ushauri wasiliana nami mi zee la mjini kwa wanawake tu
humbleforeal@rocketmail.com
Upendo  - Housewife   |80.72.99.xxx |2010-01-10 08:57:07
Ni kweli ila maisha yamebadilika sana,
na wanaume wanachoka sana wanahitaji
kushtuliwa / kuchokozwa na wamama.
Tusikae kimya lazima tuchangamke!!!
Diwani  - Inabidi wanawake Wajitume...   |196.41.60.xxx |2010-01-13 05:21:24
Unajua hili suala ni zito zaid ya watu wanavyolifikiria kwani inahitajika busara
nyingi kuweza kutambua...Tatizo wanawake wa sasa au wa kipindi hiki huwa
hawajitumi hasa wakiwa kwenye bed yaani wanalala kama magogo..... Inatakiwa
wajue vionjo vingi vitakavyowapendeza wenza wao na waelewe huu si wakati wa
kuoneana aibu...Inabidi wajue alot of styles....and that styles will help them
to develop their NDOA....Hivi wewe dada ukivaa kanga moja halafu ikiwa imeloana
na vijimaji waona hatari? Jitumeni jamani...kukatika peke yake haitoshi kumvutia
mume katika chakula cha usiku...UBUNIFU NDIO UNAHITAJIKA.....Hakuna porojo wala
utani katika suala la chakula cha usiku..Ieleweke ma SISTER DU NDIO MARA NYINGI
WANAKUWA WA KWANZA KUACHIKA hiyo yote ni kutokana na kupeleka U Sister kwenye
mambo ya msosi wa usiku...NATUMAINI SITOKUWA ADUI WENU KWA KUSEMA UKWELI....
Theo  - wanaume wanatoka sana nje ya ndoa   |80.254.146.xxx |2010-02-18 01:16:41
kwa mtazamo wangu wanamake huwa wanakuwa waaminifu sana na commited once
wanapoingia kwenye ndoa so the only place anayosubiri chakula cha usiku ni kwa
mumewe tu,but kwa ndugu zetu inasikitisha jinsi wanavyotekwa kirahisi na
kujikuta wanatoka sana nje ya ndoa.obvious akifika kwako atakuwa kachoka analala
wakati we una kiu unamsubiri.fumbueni macho!!!!!!!!
mimi  - chakula cha usiku   |41.221.50.xxx |2010-03-03 04:01:29
duu hii kali tunashukuru maana sisi wengine kwenye ndoa bado hatujaingia but
tunafikili mambo yanakuwa bado mukide hata ndani ya ndoa thanx........
shasu  - baba mtu   |196.44.162.xxx |2010-03-06 06:05:24
Mimi nafikiri pia mazingira tunayoishi sasa hivi yanachangia wanaume kutowapa
wake zao chakula cha usiku vile ipasavyo. Zamani ilikuwa ni nadra sana kukuta
mwanamke akionyesha baadhi ya maungo yake (sehemu za mwili wake). Lakini sasa
hivi (wakati huu tulionao) imekuwa ni mtindo kwa wanawake kuonyesha sehemu za
miili yao, wenyewe wanasema wanakwenda na wakati. Hivyo mchana kutwa mwanamume
anashinda akitazama nyuchi (sehemu za wanawake zinazoachwa wazi), iwe ofisin au
njiani. Hali hii inamfanya mwanamume huyu kupoteza hamu ya kutoa chakula cha
usiku kwa mkewe pindi arudipo nyumbani kwani hamu inakuwa imekwisha kwa kutazama
maungo ya wanawake huko njiani. Mwanamume asipozoea kuonaona maungo ya mwanamke
anakuwa na hamu ya kutoa chakula cha usiku kwa mkewe.
jitu la miraba minne.  - chakula cha usiku   |57.67.135.xxx |2010-03-19 07:07:19
Nimekukubali sana baba mtu.ingawa wtu wanaweza wasilichukulie uzito sual
hili.lakini linachangia sana.bigiee up shashu kwa kuona mbali.
mukulu wa nzukulu  - msosi wa night   |80.72.96.xxx |2010-03-26 02:47:20
nakubaliana sana na shasu-baba mtu a.k.a mzee wa nyuchi, ila kwa kuongezea, hawa
dada zetu wanalalamika sana ila ukichunguza kwa makini hizi ndoa za sasa
zimekuwa fashion, wanataka kuolewa ili jamii iwatambue na kwa sifa bila ya kujua
majukumu yao ya ndani wanamokwenda!!!! muandalie mazingira mazuri ya msosi na
utamuona nyumbani hata kabla ya muda wa kazi kuisha!!!!!
Tea Cake  - Researcher   |196.45.158.xxx |2010-05-23 23:39:33
Aaaaawapi hamna lolote ni kuchokana na kuchukuliana poa tu watu wanakua
wameishiwa upendo miongoni mwao baada ya kuishi kwa muda mrefu! mbona partner
mpya mtu anakua anajitahidi kujituma kufanya nae mawasiliano, care hata ktk
hicho chakula iweje baada ya miaka ndo uwe bize, wizi mtupu hata mimi demu wangu
nshamchoka sina mzuka nae tena hata nisipofanya nae miezi poa tu....semeni
ukweli wadau sio mnajizungushazungusha!!!
shasu  - baba mtu   |196.44.161.xxx |2010-06-17 03:27:43
kwako unayejiita TEA CAKE-Researcher
Inaonekana una matatizo. Naomba usome tema
hayo maoni huenda ukaelewa. Inakuwaje umemchoka dem wako????!!!!!
Inawezekana
unaumwa au ni mtu wa macho juu, kila ukiona dem unamtamani na kumuona ni mzuri
kuliko ulo naye. Usiuendekeze moyo unavyokutuma, kwani unadanganya, jaribu
kushinda, na usiposhinda utakuja kuumia na kujivika kitanzi pasipo huruma.
Kuishi muda mrefu sio sababu ya kumchoka mwenzio. Inatakiwa mbadili staili ya
kula chakula cha usiku. Usikariri kuwa mlo wa usiku siku zote ni wali
mchuzi/maharage. Siku moja moja mnaweza mkala ndizi au tambi au chapati mchuzi
na maisha yakasonga mbele kama kawa na hutamchoka mpishi.
Inawezekana tayari ni
muhathirika wa yale nlosema, kuwa unaona nyuchi nyingi za wanawake wengine
mchana kutwa hali inopelekea usiwe na mzuka na dem wako
beatrice  - wafaham kuwa....?!   |82.206.128.xxx |2010-06-15 08:29:11
jamani chakula cha usiku isiwe kutimiza wajibu tu, nikumpa mwenzi wako cha
ukweli. mambo yote ni kuongea na kuelewana, wanawake tujifunze kuwa wawazi kwa
waume wetu, sio chakula tu ila umwambie unataka chakula kiweje, kipikweje,
kigeuzejwe n.k. swala la mazoezi ni muhimu, tuangalie aina ya vyakula
tunavyokula maofisini, tuweke mipaka katika kazi ili tupunguze stress
tusizipeleke majumbani kwetu; nani alikwambia ukiwa na pesa nyingi, au ukifanya
kazi sana ndo maisha bwana!!na tupunguze kutazama vijisketi makazin na
vijisuruali. tafuta pesa kiasi na mridhishane
shasu   |196.44.161.xxx |2010-06-17 03:52:14
Asante shost beatrice kwa kuuona ukweli. Ni kweli kabisa kuwa wanawake wengi sio
wakweli katika suala zima la chakula cha usiku. Wanawake wengi huwa hawasemi ni
aina gani ya chakula kiliwe usiku, na kipikwe vipi. Wenyewe wasubiri mume atoe
maagizo kisha wao hufuata. Kuna wanawake wengine hawasemi kabisa kuwa njaa
zinawauma hivyo wanahitaji mlo wa usiku. Linapokuja suala la chakula cha usiku,
inatakiwa mvunje ukimya. Mwanamke anatakiwa ajue kuwa kupata chakula cha usiku
ni haki yake, asipopewa anapaswa adai. Na mwanamme ni vivyo hivyo. Maumbile yetu
pia yana nafasi yake katika suala zimala chakula usiku.
Write comment
Name:
Email:
 
Title:
UBBCode:
[b] [i] [u] [url] [quote] [code] [img] 
 
 
Please input the anti-spam code that you can read in the image.

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Habari Motomoto

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20

Login Form