***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
Jaji Kiongozi, Salum Masati, wa Mahakama Kuu ya Tanzania akisoma hukumu leo iliyochukuwa masaa sita, amewaachia huru washtakiwa wote wa kesi hiyo ya mauaji.
Katika kesi hiyo, Zombe na wenzake walikuwa wakituhumiwa kuwaua wafanya biashara wa madini Ephraim Sabinus Chigumbi, Sabinus Chigumbi (Jongo), Mathias Lung’ombe na Juma Ndugu aliyekuwa dereva teksi na mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Januari 14, mwaka 2006 katika msitu wa Pande, Mbezi Luisi wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Akisoma hukumu hiyo leo Jaji Masati alisema kuwa washtakiwa wote hawana hatia kwakuwa hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaonesha kuwa watuhumiwa hao walihusika katika kufanya mauaji ya wafanyabiashara hao.
Jaji Masati amesema kuwa amekosa ushahidi wa kuwatia hatiani pamoja na kusikilizwa kwa mashahidi wote 37.
Katika kesi hiyo iliyosikilizwa zaidi ya miaka miwili, jumla ya mashahidi 37 walifika mahakamani katika siku tofauti tofauti kutoa ushahidi juu ya mauaji hayo.
Washtakiwa katika kesi hiyo walikuwa ni Abdallah Zombe ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Bageni, Makele, WP 4513 Jane, D1406 Mabula, D8289 Michael, D2300 Abeneth, B1321 Rashid, D4656 Rajab na D1367 Philipo.
Mshitakiwa Lema alifutiwa kesi baada ya kufariki dunia kutokana na kusumbuliwa na maradhi akiwa gerezani ambapo alilazwa katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road.
Baada ya kusomwa kwa hukumu hiyo baadhi ya mamia ya watu waliojazana ndani na nje ya mahakama walionekana kutoridhishwa na hukumu hiyo.
Mtuhumiwa pekee wa kike katika kesi hiyo WP 4513 Jane, alizirai baada ya hukumu ya kesi hiyo kusomwa , hivyo kufanya apakizwe kwenye gari la wagonjwa "ambulance" na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata huduma ya kwanza.
PICHA HIZI HAPA
ni kicheko wakati ACP Abdallah Zombe na wenzie wakiwa wamezungukwa na makachero na wanahabari wanaondoka mahakama kuu kupitia mlango wa nyuma mara baada ya mahakama kuwaona hawana hatia kwa mashitaka ya mauaji ya wafanyabiashara wa mahenge baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha tuhuma hizo
umati mkuwa wa wadau ulijaa hadi nje ya jengo la mahakama kuu
wakili machachari aliyemtetea zombe Mh. Jerome Msemwa, akipewa hongera wakati yeye na timu yake wakiondoka mahakama kuu baada ya kuigalagaza timu ya upande wa mashitaka
washtakiwa wakiwahi kudandia farasi mweupe baada ya kuchoropoka
zombe akidandia vitara iliyokuja kumchukua
wadau wakiwa wameachiwa vumbi na vitara aliyopanda zombe
mahakama kuu palikuwa hapatoshi
zombe huyoooo anakitoa huku mashabiki wake wakiimba zombe! zombe! zombe!!
Wakili wa Upande wa Serikali Jasson Kashozi akihojiwa na wanahabari mwara baada ya hukumu ya Zombe na waenzake 9 ambao wameachiwa huru na mahakama kuu baada ya kutopatikana na hatia jioni hii kutokana na mashitaka ya mauaji ya wafanyabiashara watatu iliyokuwa ikiwakabili.
| Comments |
|
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Habari Motomoto
-
Wahariri kujadili jinsi ya kuwasaidia wapiga kura wakati wa kampeni Wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini watakutana jijini...
-
Slaa apata mapokezi makubwa Musoma, Mwanza Maelfu ya wananchi, wakiwamo watumishi wa serikali, wafanyabiashara...
-
Jaji Mkuu: Hatukushinikizwa hukumu ya mgombea binafsi Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustine Ramadhan, amesema uamuzi wa Mahakama...
-
Ajali ya basi yaua abiria 16 Watu 16 wamefariki dunia na wengine 48 kujeruhiwa baada ya basi la...
-
Kura ya maoni Z`bar yamg`oa DC Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amemfukuza kazi Mkuu wa Wilaya...
-
Takukuru sasa inatawala nchi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imewakamata makada...
-
Karume awa mbogo Z`bar Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, amevunja ukimya kwa kusema kuwa...
-
Umati wamlaki Slaa jijini Arusha Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod...
-
Jaji Eliamani Mbise afariki dunia Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Eliamani Mbise, amefariki dunia...
-
Tume ya uchaguzi yataka ushahidi wizi wa kura Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeomba kupewa taarifa za mianya ya wizi...
-
Waibuka washindi Viti Maalum CCM Wagombea kadha wameibuka na ushindi katika mchuano wa kura za uteuzi...
-
Waziri Sitta azungumzia sakata ya Takukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Magreth Sitta, amekanusha...
-
Kamanda Takukuru ashushwa cheo WAKATI habari za rushwa zikiendelea kutawala harakati za kuwania ...
- 1
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6
- 7
- 8
- 9
- 10
- 11
- 12
- 13
- 14
- 15
- 16
- 17
- 18
- 19
- 20
Zilizosomwa Sana
- Schorlaships
- MAJINA YA WANAFUNZI 33658 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, VYUO VYA UFUNDI NA CHUO CHA MAJI MWAKA 2010
- United States
- CHAKULA CHA USIKU: WAHANGA SASA NI WANAWAKE! - Mwambie, usione haya
- AFYA! AFYA! Mambo yote muhimu haya hapa
- Dawa za Kuongeza Ufanisi wa Mwanaume Kitandani Zazinduliwa
- Europe
- Advertisement Plan
- ***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***
- Aliyefumwa akibaka bintiye ala kichapo
- Australia
- Man Utd ushindi sasa basi
- Wanafunzi walioteketea kuzikwa kaburi moja leo
- Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi
- United Kingdom
- Henry Joseph Shindika aula

